Akiorodhesha mifano kadhaa iliyotokea tangu kumalizika kwa uchaguzi mkuu uliopita, Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, ameituhumu Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) chini ya uongozi wa Dk. Ali Mohammed Shein kwa kuendesha nchi kwa misingi ya ubaguzi wa uzawa na uvyama. Hayo ameyasema leo Chake Chake kisiwani Pemba, ambako ameanza ziara yake ya wilaya nne kichama.
↧