Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendelea (CHADEMA), Freeman Mbowe, amesema kuwa wananchi wanaushinikiza uongozi wa chama hicho kuwaruhusu kutumia njia zao wenyewe kujilinda na kulipiza kisasi dhidi ya mauaji na mateso yanayofanywa kwao kutokana na sababu za kisiasa, lakini yeye na viongozi wenzake wanawazuwia kwa kuwa wanaamini kwenye ustaarabu na kuheshimiana.