Kama ambavyo polisi wana haki ya kukukamata kwa kufuata masharti ya kisheria, basi pia nawe una haki ya kupatiwa dhamana haraka iwezekanavyo kwa masharti hayo hayo ya kisheria. Msikilize Rais wa Chama cha Wanasheria cha Zanzibar (ZLS), Omar Said Shaaban, kwenye mfululizo huu wa Zaima Sheria.