Mwenyekiti wa Kamati ya Uongozi ya Chama cha Wananchi (CUF), Julius Mtatiro, amesema kuwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) na ile ya Zanzibar (ZEC) ndio maadui wakubwa kwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akitabiri kwamba katika siku zijazo taasisi hizo zenye dhamana ya kusimamia uchaguzi zitaiingiza nchi kwenye maafa makubwa.
↧