Miongoni mwa yaliyotanda safu za mbele za magazeti ya leo ni kashfa ya vyeti vya kughushi kwenye jeshi la polisi, uwezekano wa Tanzania kupata soko kubwa la muhogo nchini China na kuuawa kwa kiongozi mwengine wa CCM mkoani Rufiji. Kwenye kurasa za michezo, habari kuu ni tafrani kwenye klabu maarufu ya Simba, ambapo mzozo wa kile kiitwacho “SportPesa” umeanza kuwang’oa vigogo wa timu hiyo kubwa ya soka.






















