Wengi tunakubaliana kuwa uvutaji sigara ni hatari kwa afya ya mvutaji na hata waliomzunguka, kwani moshi wa tumbaku una madhara ya moja kwa moja kwa afya na hata kwa mazingira. Lakini hivi unajuwa kuwa uvutaji sigara unaweza kuwa kipaji kama vipaji vyengine walivyonavyo watu, mfano uimbaji, ushonaji na kadhalika? Kijana Michael Lee aliwashangaza majaji kwenye mashindano ya kusaka vipaji nchini Ufaransa mwaka 2016 kwa namna anavyousarifu na kuusanifu moshi wa sigara yake. Angalia vidio hapo chini lakini tahadhari sana kwani UVUTAJI SIGARA NI HATARI KWA MAISHA YAKO.
Filed under: BURUDANI
