Quantcast
Viewing all 854 articles
Browse latest View live

Uhuni huu kwenye siasa zetu haufai kuachiwa

MTU mmoja ambaye sitamtaja jina kwa sasa,  kanitumia ujumbe mfupi wa maandishi akishangilia vitendo viwili vilivyotekea kwa wakati mmoja katika siasa za nchi yetu.

Kitendo cha kwanza ni cha baadhi ya madiwani waliojivua uanachama wa Chadema na kujiunga na CCM katika mikoa ya Arusha na Kilimanjaro pamoja na sehemu nyingine ambazo bado sijazithibitisha. Kingine ni cha anayejiita mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, kuwavua uanachama wabunge 8 wa chama hicho.

Mtu huyo ambaye anajifanya mweledi wa kila kitu kuanzia usafirishaji wa majini, masuala ya kibalozi, masuala ya kodi na kadhalika, anakosa kuelewa kwamba uchochezi na uchonganishi wa kisiasa ni jambo hatari sana katika mustakabali wa nchi!

Ndiyo, mtu huyo anaweza akawa anayaelewa baadhi ya mambo kwa njia ya kukariri sawa na watoto wa madrasa wawezavyo kuihifadhi Qur’an Tukufu bila uwezo wa kuichambua. Na kwa mtaji huo hataki kukubali kwamba haijui siasa na mambo anayoyashadidia kwenye siasa ni ya hatari kabisa kwa nchi iliyodumu na amani kwa miongo mingi.

Tukianza na suala la madiwani waliovua uanachama wa Chadema na kujiunga na CCM tutaona kwamba kuna mambo kama yafuatayo. Kitendo hicho ni uasi, sio kwa chama tu bali pia kwa wananchi.

Chama kiliwaamini watu hao na kuwapeleka mbele ya wananchi kuwa ndio wanaowafaa, na wananchi wakaridhika nao kwa kuwachagua dhidi ya watu walioletwa kwao na vyama vingine.

Baada ya hapo wachaguliwa hao wakala viapo vya kuwa madiwani wakiwa wanamhusisha Mwenyezi Mungu kwa kushika vitabu vitakatifu, Qur’an na Biblia, kuwa watawatumikia wananchi waliowachagua kupitia njia walizozitumia na kuonekana wanafaa, vyama vya siasa.

Kwahiyo tutaona kwamba kuziruka njia hizo na kuzidandia njia nyingine sio tu kwamba wameziasi na kuzisaliti njia hizo, bali pia wamemuasi na kumsaliti Mungu waliyemuomba awasaidie katika majukumu yao hayo ya kuwatumikia wananchi,  ikiwa ni pamoja na kuwaasi na kuwasaliti wananchi waliowachagua kwa ujumla.

Kitendo hicho cha kukiasi kiapo cha aina hiyo ni zaidi ya usaliti, ni kitendo ambacho ni aina mojawapo ya uhaini. Uhaini ni uovu uliopitiliza kutokana na kuyabadili matakwa ya wananchi yanayolindwa na kiapo chini ya Katiba ya nchi.

Kwa hiyo, yeyote anayekishangilia kitendo hicho, hata awe mchumia tumbo tu, mtu asiyejari kinachoweza kutokea ilmradi tu yeye kajaza tumbo lake, anapaswa achukuliwe kama mtu kipofu asiyepaona anakoelekea. Na mtu wa aina hiyo ni hatari sana katika jamii. Maana kwa mtindo huo asiposhituliwa na kukemewa anaweza akaiingiza jamii nzima kwenye gema na kuisababishia maangamizi.

Nasema hivyo nikiwa nimetilia maanani kitendo cha kuapisha, sababu kazi yoyote isiyo ya maana haiwezi kuhitaji uapishwaji. Lengo kuu la kuapisha ni la kumtaka mhusika asilete uasi na usaliti, ili kuwafanya waliompa kazi husika wamuamini.

Kwa hiyo, anayekiuka kiapo na kujiingiza kwenye uasi na usaliti anawezaje kuaminika kwenye jamii aliyomo? Madiwani hao waliojivua uwakilishi wa wananchi wakidhani wanakikomoa chama kilichowasimamia mbele ya wananchi wanawezaje kuaminika kokote waendako?

Hivi kweli CCM inaweza kuwaona hao kuwa ni watu safi au ni ng’ombe waliokatika mikia kama alivyowahi kusema mwenyekiti wao, Dk. Jonh Pombe Magufuli? Kwa mantiki hiyo, tayari hao ni watu wasiofaa, sio kwa wananchi peke yao, hata ndani ya CCM watu hao hawafai kabisa, maana alishaliona hilo mwenyekiti wa chama hicho.

Kwa upande mwingine, ni wabunge 8 waliovuliwa uanachama na anayejiita mwenyekiti wa CUF, Profesa Lipumba. Kitendo alichokifanya profesa huyo kinajionesha wazi kilivyo cha usaliti, sio kwa wabunge hao tu, bali pia kwa CUF, upinzani nchini na taifa kwa ujumla.

Sababu kitendo hicho kinaziweka wazi nafasi za wabunge hao, maana yake ni kwamba zikajazwe upya. Kazi ya uchaguzi mdogo kwa ajili ya kuzijaza nafasi hizo, kama ilivyo ile ya kujaza nafasi za madiwani waliojivua uanachama wa Chadema, ni ya gharama.

Pesa itakayotumika sio ya vyama vya siasa, ni pesa ya walipakodi. Kwahiyo mtu aliye mzalendo makini alitakiwa kuliona hilo akiwa anaelewa kwamba kwa sasa nchi imo kwenye msukosuko mkubwa wa kipesa. Isingekuwa rahisi kwa mtu mzalendo kusababisha gharama kwa taifa katika jambo lenye maslahi binafsi kiasi hicho.

Sababu anachokitafuta Lipumba ni kutaka kujisimika vizuri kwenye nafasi ya uenyekiti wa CUF ambayo aliikimbia mwenyewe kiusaliti akidhani angekiyumbisha chama hicho wakati kiko kwenye harakati za Uchaguzi Mkuu wa 2015.

Lakini baada ya kuona chama hicho hakikuyumba, kwa maana ya malengo yake, Lipumba, kukwama,  ndipo akaja kivingine akidai kwamba yeye bado ni mwenyekiti wa chama hicho! Anafanya hivyo bila kujali kwamba anachezea bomu linaloweza kulipuka na kusababisha maafa makubwa kwa nchi na wananchi! Tamaa mbele mauti nyuma!

Tamaa ya maslahi binafsi aliyo nayo Lipumba inamfumba macho asiweze kuona hatari iliyo mbele yake,  kwa nchi na wananchi. Maana kama tulivyoona hapo juu, nchi itaigia gharama ya uchaguzi mdogo na pia uwezekano wa wananchi kuvurugana kwa ajili ya uchaguzi huo mdogo.

Hata kama vyombo vya dola vipo kuhakikisha hilo halitokei, bado vitahitaji gharama kubwa katika kulitekeleza hilo. Sio kwamba vyombo vya dola vinajazwa upepo tu na kuanza kufanya kazi.

Mtu aliyenishangaza zaidi ni Spika wa Bunge, Job Ndugai,  kuwahi kuridhia hatua hiyo ya Lipumba na kutangaza kuwa nafasi hizo za wabunge ziko wazi. Mbona hakufanya hivyo kwa Magdalena Sakaya ambaye naye alikuwa amevuliwa uanachama wa CUF?

TANBIHI: Makala hii imeandikwa na Prudence Karugendo. Anapatikana kwa anwani ya barua-pepe prudencekarugendo@yahoo.com na kwa simu nambari 0784989512

 


Filed under: SIASA Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Kuimaliza CUF ni kuimaliza Zanzibar

Kikiwa kama chama kikubwa cha kitaifa, Chama cha Wananchi (CUF) kinafanana na vyama vingine vingi vya kisiasa ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, lakini kina jambo moja kubwa ambalo kimejipambanuwa kutoka vyama vyenziwe. Nalo ni falsafa yake juu ya nafasi ya Zanzibar kwenye Muungano huo.

Hiki ni chama pekee kilichojikita kwenye “Siasa za Muungano” kama mtaji wake mkuu wa kisiasa upande wa Zanzibar. Hakuna chama chengine chochote ambacho kina dira ya kuifanya Zanzibar kuwa mshirika mwenye nguvu za kweli ndani ya Muungano huu kama ilivyo CUF.

Na hapa ndipo tatizo lenyewe lilipo. Siasa za Muungano. Zile ambazo zinasema kuwa “ili uwe na Muungano imara basi lazima uwe na Zanzibar dhaifu” na ambazo zinaiona Zanzibar imara kama jambo hatari kwa Muungano huo.

Kwa waumini wa siasa hizo za Muungano, chochote kinachoipa Zanzibar taswira ya uimara ni kitu cha kuchukiza na kisicho na uhalali wa kuishi. Kinapaswa kuangamizwa mara moja, tena kwa kadiri ambavyo inawezekana.

Hiki kinachoendelea sasa hivi dhidi ya CUF kina mashiko yake kwenye ukweli huu wa utekelezaji wa siasa za Muungano kuelekea Zanzibar.

Kwa muda wote, tangu kuanzishwa kwake mwaka 1992, CUF imekuwa mwiba mbaya kooni mwa waumini wa siasa hizo za Muungano walio ndani na nje ya visiwa vya Zanzibar.

Waumini hao hasa ni watiifu kwa makao makuu ya siasa zenyewe, Chimwaga, na ambao kwa hakika hasa sio kwamba wanaupenda Muungano kama Muungano, bali wanaupenda Muungano ule ambao kwawo, nchi moja iko juu ya nyengine kisiasa, kiuchumi na kijamii.

Waumini wa siasa hizo wametekeleza hujuma kubwa kubwa dhidi ya Zanzibar kabla ya Muungano wa 1964 na tangu siku za awali kabisa za Muungano wenyewe, mara tu baada ya Mzee Abeid Karume kung’amuwa mtego alionasishwa na mwasisi mwenzake wa Muungano huu.

Tangu awamu hiyo ya kwanza, takribani hakuna kipindi kilichopita salama bila ya kukuta alama, taasisi au watu wanaowakilisha taswira ya nguvu za Zanzibar ndani ya Muungano wakinyakuliwa, kudunishwa, kudhalilishwa na hata kuangamizwa kabisa kabisa.

Wazalendo wa Kizanzibari waliokuwa wasomi na wenye fikra nzito nzito za kimageuzi kutoka pande zote za ushindani wa kisiasa visiwani Zanzibar, akina Ali Muhsin Barwani, Amani Thani, Abdulrahman Mohamed Babu, Abdallah Kassim Hanga, Kanali Ali Mahfoudh, Salim Ahmed Salim, na wengine kadhaa walijikuta wakimezwa ndani ya tumbo la Tanganyika na kisha ama kuselelea huko ama kuangamia kupitia mkono wa huko.

Katika kitabu chake cha Pan-Africanism or Pragmatism? Lessons of Tanganyika-Zanzibar Union, Profesa Issa G. Shivji anazungumzia mzozo mkubwa uliokuwepo kati ya Mzee Karume na Mwalimu Julius Nyerere, hata kabla ya wino wa sahihi kwenye Makubaliano ya Muungano haujakauka.

Katika siku za mwisho mwisho za uhai wake, Mzee Karume alikuwa hazungumzi moja kwa moja na Mwalimu Nyerere na hata panapokuwa na jambo la wawili hao kuzungumzwa, lilipaswa kupitishwa kwa mawaziri wao waandamizi.

Mwisho, Aprili 1972, akiwa kama alama ya nguvu ya Zanzibar kwenye Muungano, maisha ya Mzee Karume yakakatishwa, huku maswali kuhusu wahusika wa mauaji hayo hadi leo yakibakia bila majibu, lakini tuhuma kwamba msimamo wake kuhusu Muungano ulichangia kifo hicho, zipo miongoni mwa Wazanzibari.

Miaka mitano baada ya kuuawa kwa Mzee Karume, taasisi imara kabisa iliyowasilisha na kuwakilisha nguvu za Zanzibar, chama cha Afro-Shiraz (ASP), nacho kikauliwa kwa maslahi ya kuundwa Chama cha Mapinduzi (CCM) kilichotokana na chenye nguvu zake upande wa Tanganyika.

Baada ya hujuma hii ya kuimaliza ASP kufanikiwa, hapakuwa tena na mpaka wa kukichukuwa kila kilichomo Zanzibar, iwe taasisi, mtu au alama inayoashiria nguvu za Zanzibar ndani ya Muungano. Kuanzia maamuzi hadi utekelezaji.

Ndicho kilichomkumba Marehemu Mzee Aboud Jumbe Mwinyi kwa kuvuliwa nafasi zake zote za uongozi wa kichama na kiserikali na hatimaye naye maisha yake yakamalizikia akiwa kapotezwa kabisa kwenye ramani ya siasa za nchi.

Ndicho kilichokuja baadaye kuwakumba vijana wa wakati huo ambao walikuwa alama ya nguvu ya Zanzibar ndani ya Muungano, akina Seif Sharif Hamad, Hamad Rashid Mohamed, Soud Yussuf Mgeni, Juma Ngwali, Maulid Makame, Shaaban Khamis Mloo, Juma Duni Haji na wenzao, ambao sio tu kuwa walivuliwa nyadhifa zao bali pia waliwekwa jela.

Mwanzoni kabisa, mara tu baada ya Katibu Mkuu wa sasa wa CUF, Maalim Seif, kutoka kizuizini alikokuwa amewekwa baina ya Mei 1989 na Novemba 1991, alikutana na Mwalimu Nyerere katika kile kilichoitwa “mazungumzo ya siri ya Msasani.”

Ingawa hakuna hata mmoja aliyekisema hasa walichokizungumza wawili hao, lakini inasemekana kuwa Mwalimu Nyerere alimuambia Maalim Seif kuwa afanye afanyavyo kwenye siasa zake, lakini kamwe asije akathubutu kuugusa Muungano, akimtishia kuwa akiuchezea Muungano “asingelibaki salama!”

Lakini Maalim Seif na CUF yake, inaonekana, hawakutaka kumkubalia Mwalimu Nyerere. Waliendelea kuugusa Muungano, nao wakaendelea kukabiliana na adhabu za kuugusa huko.

Miongoni mwa adhabu hizo ni mauaji ya Januari 2001, ambapo kwa mujibu wa ripoti ya shirika la haki za binaadamu la Human Rights Watch iliyopewa jina la “Risasi Zilinyesha Kama Mvua”, mashuhuda wanasema wauaji, watesaji na wabakaji wao walikuwa wakirejelea kauli za kisiasa zinazohusiana na upinzani wa wana-CUF dhidi ya Muungano.

Kwa hivyo, hata maandamano yale kwa watawala ilikuwa ni alama ya Wazanzibari kuinuka dhidi ya Muungano na yalipaswa kuangamizwa kwa namna yoyote.

Hapo katikati, kuanzia mwaka 2009, Zanzibar ilianza tena kurudi kwenye siasa za umma dhidi ya mfumo uliopo wa Muungano, ambazo zilichangiwa pakubwa na Maridhiano yaliyoasisiwa na Rais Amani Karume na Maalim Seif.

Kwa Maridhiano hayo, Kura ya Maoni ya Julai 31 ikaamuwa kuundwa kwa serikali ya umoja wa kitaifa, pamoja na Mabadiliko ya Katiba yaliyoitangaza rasmi Zanzibar kuwa ni nchi.

Yote haya yalikuwa ni alama za ukaidi dhidi ya siasa za Muungano. Ishara za kuipa nguvu Zanzibar. Asasi huru za kijamii, kama vile Jukwaa la Katiba la Zanzibar na Jumuiya ya Uamsho na Mihadhara ya Kiislamu (Uamsho), zikapata uhuru wa kuelezea hayo kinagaubaga, lakini kila mtu anafahamu yaliyowakumba viongozi wake ambao wamebambikiziwa kesi za ugaidi kwa mwaka wa nne sasa.

Ukweli kwamba uchaguzi wa Oktoba 2015 ulichafuliwa, na ambao CUF unadai kushinda na jumuiya huru za ndani na nje ya nchi zinasema ulikuwa huru na wa haki zaidi kuwahi kutokea visiwani Zanzibar, una mahusiano ya moja kwa moja na siasa za Muungano kuelekea Zanzibar na msimamo wa CUF kuelekea Muungano huo.

Kwa hivyo, hivi leo kwamba CUF imeingizwa kwenye mzozo mkubwa kabisa wa kiuongozi, ambapo kundi linalosaidiwa kwa hali na mali na vyombo vya dola linaendesha hujuma za waziwazi zinazotishia uhai wa chama hicho, ni kwa kuwa chama hicho kimesimama kama alama ya Zanzibar imara ndani ya Muungano.

Alama hii ikiachiwa nayo kwenda, kama ambavyo alama nyengine huko nyuma zimewachiwa kwenda, itaongezea idadi kwenye orodha ya maangamizi kwa Zanzibar.

Kuiangamiza Zanzibar kama nchi na kama mshirika muhimu wa Muungano ni hatua muhimu kuelekea ile sera ya “serikali moja, nchi moja, chama kimoja.”

TANBIHI: Makala hii ilichapishwa kwa mara ya kwanza na gazeti la MwanaHalisi la tarehe 31 Julai 2017


Filed under: KALAMU YA GHASSANI Tagged: Abeid Karume, cuf, Julius Nyerere, Maalim Seif Sharif Hamad, Muungano, Tanzania, Zanzibar Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Wanasheria Zanzibar sasa kusaka njia kujitoa Muungano

Kamati ya manasheria mashuhuri wa Zanzibar ina dhumuni la kusimamia mpaka kufanikiwa kwa madai ya wazanzibari ya kurejeshewa:

• Mamlaka Kamili ya Zanzibar (Sovereign Zanzibar)
• Katiba Mpya ya kidemokresia halisi, Utawala Bora na Haki za Binadam
• Mipango ya maendeleo ya uchumi na ustawi wa Wazanzibari wote bila ya ubaguzi wa aina yoyote

Endapo mpaka mwisho wa mwezi wa Septemba 2017 Rais wa Zanzibar,  Dokta Ali M. Shein na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hawakuitisha kura ya maoni chini wa uangalizi wa Umoja wa Mataifa itakayowauliza Wazanzibari endapo wanataka kuendelea na Muungano na Tanganyika au wanapendelea uhuru kamili wa Zanzibar.

Wazanzibari kupitia Kamati hii ya wanasheria mashuhuri wa Zanzibar watawasiliana na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa aitake Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ichukue hatua muafaka na za haraka kuiwezesha Zanzibar kukikalia kiti chake cha Umoja wa Mataifa kabla ya December 2017 ili kuirejeshea Zanzibar uhuru wake uliopotea tangu Muungano wake na Tanganyika.

Endapo Tanzania itakataa kutekeleza haya itatubidi Wazanzibari tushauriane ili tupate matlaba yetu kupitia Umoja wa Mataifa New York. Wazanzibari inawabidi wachukue hatua za haraka za kisiasa kikatiba na kisheria ili kuirejeshea Zanzibar Mamlaka Kamili kitaifa na kimataifa ili kurekibisha hali halisi tangu kuundwa kwa Muungano wa Zanzibar na Tanganyika.

Wazanzibari wanasisitiza umuhimu wa amani na utulivu mpaka Zanzibar iwe tena taifa huru kwa kupitia njia na taratibu za sheria za kimataifa na katiba ya Umoja wa Mataifa.

Taarifa hii imetolewa na Balozi Salim Said Rashid, Katibu wa Kwanza wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar – 1964


Filed under: HABARI Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Kwa nini demokrasia inakataliwa kwenye nchi duni?

NENO  demokrasia limekuwa ni mwiba mchungu kwenye nchi nyingi zilizo duni! Nchi hizi ambazo kwa kiasi kikubwa zinashindwa kujiendesha zenyewe bila kutembeza bakuli, ombaomba, kwa mataifa makubwa zimelikataa kabisa neno demokrasia ambalo kwa uharaka ni mfumo wa kuongoza nchi kwa kuwaachia wananchi wajiamlie majaaliwa ya nchi zao.
 
Bara la Afrika, ambalo ndilo linaloongoza duniani kwa kuwa na nchi ombaomba, kiasi cha kuitwa jina la kebehi la dunia ya tatu, ndilo linaloongoza vilevile kwa kuikataa demokrasia pasipo kutafakari kuwa hicho kinaweza kuwa ndicho kisababishi cha hali hiyo ya uduni.
 
Kimaumbile bara la Afrika ni tajiri sana kuliko mabara mengine, lakini ukosefu wa demokrasia unajionesha kuwa kirusi kikubwa kinachosababisha ugonjwa wa uduni na ufukara wa bara hili.
 
Hilo linatokana na watawala walio wengi katika bara hili kutopenda kuwashirikisha wananchi kimaamuzi kwenye majaaliwa ya nchi zao kuhusiana na utajiri zilionao. Mara nyingi, kutokana na ukosekano wa demokrasia, utajiri wa nchi unaishia kuwa utajiri wa watawala hasa kiongozi mkuu.
 
Mfano mzuri ni wa nchi ya DRC iliyowahi kujulikana kama Zaire. Nchi hiyo imejaaliwa utajiri mwingi sana ambao lakini umeishia kuwanufaisha watawala tu wa nchi hiyo huku nchi na wananchi wakibaki kwenye dimbwi la umasikini unaonuka.
 
Enzi za kiongozi wa nchi hiyo, Mobutu Sese Seko Kuku Ngbendu wa Zabanga, liliwahi kuulizwa swali kupitia kipindi cha Klabu ya Maarifa cha BBC likiuliza ni rais gani tajiri kuliko wote duniani, jibu lake lilikuwa ni Mobutu!
 
Maana yake ni kwamba utajiri wote wa Zaire ya wakati huo ulikuwa ni wa Mobutu! Marais wa mataifa yote matajiri duniani, kama Marekani, Ufaransa, Ujerumani na mengineyo hawakuwa lolote kwa Mobutu!
 
Pamoja na mataifa hayo kuhangaikia umasikini wa Zaire marais wa nchi hizo hawakuwa lolote kwa rais wa nchi waliyokuwa wakihangaika kuisaidia! Walikuwa masikini sana kwake!
 
Ni wazi kwamba ukosefu wa demokrasia nchini Zaire ndio uliomsaidia Mobutu, rais wa nchi masikini sana kuwa kinara wa ukwasi kwa marais hao wa mataifa tajiri sana duniani.
 
Kwa upande mwingine tutaona kwamba nchi ya Zimbabwe, kipindi inaitwa Rhodesia, ilikaliwa na walowezi wa Kingereza kwa muda mrefu.
 
Wananchi wazalendo wa nchi hiyo wakapigana kufa na kupona, sababu mojawapo kuu ikiwa ni kuipata demokrasia ambayo ingewawezesha kufanya maamuzi juu ya majaaliwa ya nchi yao. Ikafikia kipindi walowezi wakanyoosha mikono, hiyo ni mwaka 1980.
 
Lakini badala ya demokrasia iliyotafutwa kwa udi na uvumba Wazimbabwe wakaishia kumpata Robert Gabriel Mugabe. Yanayofanywa na Mugabe nchini humo kwa sasa hayana tofauti na yaliyokuwa yakifanywa na Ian Douglas Smith, kiongozi wa walowezi.
 
Wakati Smith hakutaka wananchi wazalendo walio wengi washiriki kwenye demokrasia, hakihofia wingi wao kumuangusha katika kuutafuta mustakabari mwema wa nchi yao, Mugabe hataki wazalendo walewale wapige kura ya kumkataa.
 
Hiyo inajionesha kwamba kuwalazimisha watu wapige kula ya matakwa yake haina tofauti na kuwazuia kupiga kura. Ni bora kuwazuia kupiga kura kuliko kuwalazimisha kupiga kura dhidi ya matakwa yao.
 
Kama tunakumbuka tutaona kwamba Zimbabwe ya Ian Smith, Rhodesia wakati huo, ilikuwa imenawili sana kulinganisha na Zimbabwe ya wakati huu chini ya Mugabe. Ndiyo maana mara tu baada ya walowezi kung’olewa Zimbabwe  ilianza kutoa misaada kemkemu kwa Tanzania kikiwemo chakula.
 
Lakini Zimbabwe ya wakati huu imedhoofika sana kiasi kwamba utakuwa ni muujiza kusikia ikitoa msaada wa aina yoyote.
 
Wakati hali ikiwa hivyo, rais wa nchi hiyo, Robert Mugabe, bado ni mmojawapo wa marais tajiri sana duniani kiasi cha hivi majuzi kutoa dola 60,000 kama zawadi ya siku ya kuzaliwa kwa shemeji yake Junior Gumbochuma!
 
Kitu cha aina hiyo hakikuwahi kufanywa na Ian Smith, yeye alitaka utajiri wa Zimbabwe uinufaishe Zimbabwe na sio kuwanufaisha tu mashemeji na ndugu wa karibu kama tunavyoona kwa sasa kwa kiongozi aliyesadikika ndiye  mzalendo wa nchi hiyo.
 
Kwahiyo kwa kiasi kikubwa ni kweli kwamba demokrasia inaogopwa katika nchi duni kwa vile inaelekea kuyaondoa maslahi mikononi mwa wachache, hasa watawala, na kuyaweka mikononi mwa umma kitu kinachoonekana kuwakera watawala walio wengi.
 
Yapo maneno yanayosemwa kinyemela, kwamba kiongozi fulani kafanya vizuri kwenye uongozi wake hivyo anasitahili kuendelea kupewa nafasi yakuongoza kinyume na matakwa ya muongozo wa nchi, Katiba.
 
Maneno ya aina hiyo yanasikika sana kwenye nchi hizi duni, haijawahi kutokea kwenye nchi tajiri, ambazo kwa lugha nyingine tunaziita nchi zilizoendelea, kwamba kiongozi aliyefanya makubwa na mazuri aendelee kuongoza kinyume cha Katiba ya nchi yake.
 
Ieleweke kwamba uzuri wa kwanza wa kiongozi, hapa nitoe mfano wa rais, ni kuuheshimu utaratibu alioapa kuulinda. Rais anaapa kulinda Katiba ya nchi. Haijawahi kutokea rais akaapa kuyalinda mazuri atakayofanya, sababu hayo ni mengineyo.
 
Rais anayekubali kuongezewa muda wa uongozi, hata awe amefanya kitu gani, hapaswi kuonekana ni rais bora. Sababu anakuwa amekiuka kiapo chake, historia inapaswa kumchukulia mtu wa aina hiyo kama kiongozi aliyekuwa hafai hata kidogo.
 
Nchi kubwa na tajiri sana duniani, Marekani, inakuwa hivi ilivyo kutokana na kuiheshimu demokrasia na Katiba yake. Haijawahi kushawishika kuibadili Katiba kutokana na uzuri wa rais anayekuwepo.
 
Wamepita marais wengi wazuri kama kina George Washington, Abraham Lincolin, Theodore Roosevelt, Franklin Pierce, JFK, Bill Clinton, Barack Obama na wengineo, lakini Katiba ya nchi hiyo haikubadilishwa ili waendelee kutawala.
 
Tuiheshimu demokrasia kwa mustakabari mwema wa nchi zetu.
TANBIHI: Makala hii imeandikwa na Prudence Karugendo anayepatikana kwa anwani ya barua-pepe prudencekarugendo@yahoo.com na simu nambari +255 784 989 512

Filed under: SIASA Tagged: demokrasia, kura, nchi, taifa Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

La uwanachama wa CAF, Zanzibar na udhaifu wa ndani

Makala hii inazungumzia kadhia ya Zanzibar kuondolewa kwenye uwanachama wake iliokaa nao siku 128 katika Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) kwa kugusia mule makala iliyotangulia ilimopitia, yaani “Siasa za Muungano kuelekea Zanzibar”, lakini kwa hoja kuwa siasa hizo za Muungano zinafanikishwa na uadui mkubwa uliomo ndani ya Zanzibar yenyewe.

Nitapiga mfano wa namna ambavyo siasa hizi zinaposhindwa kufanya kazi muda wowote ambao uadui huo ndani ya Zanzibar umedhibitiwa, na Zanzibar ikasimama kama moja kwenye mambo fulani makhsusi.

Kwa sababu ya suala lenyewe la michezo na kwa sababu ya historia yangu kwenye sekta ya utalii na vile vile kwamba kwa muda mrefu, Zanzibar imekuwa ikiunganisha mambo haya pamoja – yaani utalii, utamaduni na michezo, mfano wangu utaanguukia hapo.

Baina ya mwaka 2001 na 2010, nilikuwa mwajiriwa wa kampuni moja ya utalii visiwani Zanzibar, nilikoanzia kama mtembezaji wageni na kupanda ngazi hadi mwakilishi wa kampuni hiyo kwenye hoteli za mashariki mwa kisiwa cha Unguja.

Mwezi Machi 2008 ulikuwa muda mwengine wa kufanyika maonesho ya kimataifa ya utalii ya Berlin, Ujerumani, maarufu kama ITB. Kampuni za utalii visiwani Zanzibar kupitia chama chao (ZATO) na kwa kushirikiana kikamilifu na kamisheni ya utalii chini ya usimamizi wa wizara yenye dhamana ya utalii, wakaamuwa kushiriki kwa mara ya kwanza wakiiwakilisha Zanzibar kama Zanzibar.

Sababu moja kubwa kabisa ya makampuni hayo kutaka kwenda yenyewe kuitangaza nchi, ilikuwa ni ukweli kuwa kamwe Zanzibar haikuwahi kuuzwa kama Zanzibar na mamlaka ya utalii ya Tanzania Bara, ambayo hadi sasa inataka kujiaminisha kuwa ni mamlaka ya utalii ya Tanzania nzima.

Matokeo yake, Zanzibar ilikuwa inauzwa kwenye vifurushi vya safari za watalii barani Ulaya na Amerika kama sehemu tu ya mapumziko kwa wageni waliokwishatembelea mbuga za Tanzania Bara, na sio kama kituo kikuu cha utalii.

Kwa hakika, hata mamlaka za utalii za Kenya zilikuwa zikiiuza Zanzibar kwa mahadhi hayo hayo, kwa kuiunganisha na Mombasa. Hili lilimaanisha kuwa Zanzibar haikuwa ikipata fedha za kutosha, licha ya kuwa wageni walimiminika kwa wingi kwenye hoteli na fukwe zake.

Kwa kuyazingatia hayo, ndipo chini ya Amani Karume kama Rais wa Zanzibar na Samia Suluhu Hassan kama waziri wa utalii, biashara na uwekezaji, Zanzibar ikaamuwa kushiriki maonesho.

Kilichotokea kwenye maonesho yenyewe mwaka huo kilikuwa kituko cha mwaka, lakini ambacho inaonekana kilishatarajiwa na Wazanzibari. Maafisa usalama wa ubalozi wa Tanzania nchini Ujerumani ‘waliwavamia’ wasimamizi wa banda la maonesho la Zanzibar na kuwataka walivunje.

Hoja yao kubwa ni kwamba Zanzibar ni sehemu ya Tanzania na hivyo haikupaswa kujitangaza yenyewe kwenye maonesho hayo kama nchi. Kwamba kufanya hivyo kulikuwa ni kinyume na itifaki za kimataifa na hatari kwa Muungano wa Tanzania.

Kwa mujibu wa mmoja wa waliokuwepo kwenye banda hilo, maafisa hao wa usalama walifika mahala pa kukiita kitendo hicho cha Zanzibar kufunguwa banda lake kuwa ni sawa na ‘uhaini’.

Bahati mbaya kwa maafisa hao wa usalama kutoka ubalozini ni kwamba waliwakuta Wazanzibari wakiwa wamejitayarisha kwa lolote ambalo lingeliweza kutokezea, kwani banda halikuvunjwa hadi mwisho mwa maonesho yenyewe. Kikubwa ambacho wasimamizi wa banda hilo walikifanya, kilikuwa ni kuweka mabango ya Tanzania ndani ya banda lenyewe ili kufikia muafaka na maafisa usalama kuwa Zanzibar inabaki kuwa sehemu ya Tanzania, ingawa inaweza kujitangaza na kujiuza kama Zanzibar.

Lakini sinema hii haikuishia hapo. Mwaka 2010, wakati kampuni za utalii zinajitayarisha kwenda maonesho mengine ya ITB ya mwaka huu, mamlaka ya utalii ya Tanzania Bara ikatuma ujumbe wake visiwani Zanzibar kwenda kusaka suluhisho la hali iliyojitokeza hapo kabla.

Bado, ujumbe huo ulikuwa na kauli ile ile, kwamba Zanzibar haipaswi kujitangaza kama Zanzibar kwenye jukwaa hilo la kimataifa, kwamba kinachofanywa na Tanzania Bara kwenye maonesho kama hayo ni kwa ajili ya Tanzania nzima na kwamba, kwa hivyo, Zanzibar iwe sehemu tu inayowakilishwa na Tanzania Bara na siyo kujiwakilisha na kujitangaza yenyewe.

Nao pia, kama walivyokuwa wale maafisa wa usalama wa ubalozini mjini Berlin, walikuwa na kauli zinazofanana juu ya kampuni za utalii za Zanzibar “kuuhatarisha Muungano”. Baada ya kutoka kwenye Kamisheni ya Utalii, sasa ukawa wakati wa wajumbe hao kutoka Bara kukutana na wamiliki wa kampuni za utalii kwenye ukumbi wa hoteli ya Bwawani.

Inayumkinika kuwa, kutokana na tabia ya woga waliyonayo baadhi ya viongozi wa taasisi za serikali ya Zanzibar pale wanapokutana uso kwa uso na wenzao kutoka taasisi kama hizo kutokea Bara, huenda wakuu wa Kamisheni ya Utalii ya Zanzibar (siku hizo chini ya Katibu Mkuu Alhalil Mirza), hawakuwaambia wenzao wa Bara kwamba suala la Zanzibar kwenda ITB lilikuwa suala la serikali nzima ya Zanzibar na sio la ZATO tu.

Ndio maana, walipoanza maafisa kutoka Bara ilikuwa moja kwa moja kuwashambulia jamaa wa ZATO kwamba wanataka kuharibu nchi kwa kujipeleka kwao Ujerumani kama Zanzibar wakati Zanzibar ni sehemu ya Tanzania. Hili jamaa wa ZATO hawakuwacha lipite hivi hivi. Wakawaeleza kinagaubaga nini kilichopo na kipi kinapaswa kufanyika.

Kwamba, kwanza, utalii si jambo la Muungano, kwa hivyo Zanzibar haihitaji kuwakilishwa na Tanzania kwenye jambo ambalo si la Muungano; pili, hata kama lingelikuwa la Muungano, basi taasisi za Tanzania Bara sio taasisi za Jamhuri ya Muungano, kwa hivyo hazina haki ya kukiwakilisha cha Muungano, na tatu; hata banda ambalo Zanzibar hukodi kwenye ITB huwa linachangiwa kwa pamoja kati ya Kamisheni ya Utalii na ZATO, kwa hivyo hii ni hatua ya pande zote zinazohusika visiwani Zanzibar, na sio ya ZATO pekee.

Msimamo huu wa Bwawani 2010 ndio ambao umesalia hadi hivi leo, miaka minane baadaye. Zanzibar imeendelea kujiwakilisha kila mwaka kwenye maonesho hayo, na imekuwa ikijiuza yenyewe kwa njia zake.

Hadithi hii ya Zanzibar, ZATO na ITB ina mafunzo makubwa sana kwenye hii kadhia ya Zanzibar kuvuliwa uwanachama wa CAF. Inawezekana kuwa ni kweli kwamba, kwanza, CAF inatumia hoja ya kuwa nchi haiwezi kuwa mwanachama wake kama si mwanachama wa FIFA. Kwa hivyo, Zanzibar ilipaswa kwanza kuwa kwenye FIFA.

Pili, CAF na FIFA – kwa pamoja – zilimeelezwa  kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi moja tu na ambayo chombo chake cha uwakilishi kwenye soka ni Shirikisho la Soka la Tanzania Bara (TFF), na kwa kuwa mashirikisho hayo ya kimataifa humtambua mwakilishi mmoja kwa kila nchi, basi TFF aliyejipeleka kama mwakilishi wa Tanzania nzima, ndiyo keshajaza nafasi hiyo.

Kwenye utalii, hoja za waliokuwa hawakutaka Zanzibar ijiwakilishe na kujiuza yenyewe kimataifa zilikuwa zinafanana na hizi. Lakini tafauti ni kuwa uongozi wa juu wa serikali ya Zanzibar na kampuni za utalii, kwa pamoja, ulisimama imara kujenga hoja ya kipi ni kipi, na hivyo ndivyo ikawa.

Kwenye hili la soka pia, hoja ni zile zile ambazo zinaweza kutumiwa na Zanzibar, kwanza kwa mamlaka za ndani ya Zanzibar na Tanzania, kisha kwa mashirikisho hayo ya soka ya kimataifa, ukiacha mbali hoja nyengine zinazohusiana na undumilakuwili wa FIFA na CAF yenyewe kwenye suala hili la uwanachama wa Zanzibar.

Ni kweli kuwa siasa za Muungano zinataka kuiona Zanzibar ikiwa dhaifu ili kuweka mizani ya umadhubuti wa Muungano huo, lakini ni siasa dhaifu za ndani ya Zanzibar zenyewe ndizo hasa zinazoziruhusu siasa hizo za Muungano kufanikiwa.

TANBIHI: Makala hii ilichapishwa kwa mara ya kwanza na gazeti la MwanaHalisi la tarehe 7 Agosti 2017.


Filed under: HABARI Tagged: CAF, FIFA, Michezo, soka, utalii, Zanzibar Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Nguzo ya tatu ya mitaji ya mafanikio ni vipaji

Kila mtu aliyezaliwa hapa duniani anacho kitu pekee alichojaaliwa nacho. Si umbile lake, elimu yake, umaarufu wake, usomi wake, cheo chake katika jamii, au utajiri wake wa vitu na fedha; la hasha, ni kipaji chake. Uwezo wa kiasili ndani ya mtu katika maumbile, nafsi na roho yake huitwa kipaji. Kinatoka ndani yake. Vipaji ni tunu au zawadi toka kwa Mungu ambayo hakuna anayeweza kutunyang’anya au kutuibia mpaka tutakapokufa.

Fedha na magari vyaweza kuibiwa, nyumba inaweza kuanguka, kubomoka, kubomolewa au kuungua, lakini vipaji hubakia kuwa nasi daima. Ni kama nyuki wanavyotengeneza asali tamu na ya ubora wa viwango vya hali ya juu, lakini hawafundishwi na yeyote wala kusomea popote. Hawana stashahada wala shahada! Ni uwezo wa asili ulio ndani yao. Ndivyo vipaji vyetu vilivyo, ni kama uwezo wa nyuki ulivyo katika kuzalisha asali tamu.

Vipaji vinatofautiana baina ya watu kama ambavyo viungo vya mwili viko tofauti na kila kiungo kina kazi yake tofauti. Macho yana kazi tofuati kabisa na pua. Mikono ina kazi tofauti kabisa na masikio. Moyo una kazi tofauti na kongosho. Meno yana kazi tofuati na vidole, nk.; lakini viungo vyote hufanya kazi tofuati kwa ajili ya faida ya viungo vyote na mwili wote.

Jamii ni kama mwili, una watu tofauti wenye uwezo au vipaji tofauti kama ambavyo mwili una viungo tofauti vyenye uwezo tofuati. Watu, kama viungo vya jamii tunapaswa kutumia vipaji vyetu tofauti kwa faida ya watu wote na jamii nzima. Hilo ndilo kusudi la Mungu la kutujaalia vipaji au uwezo tofauti kwa ajili ya kutufaidisha wenyewe, kufaidiana na kuifaidisha jamii.

Kipaji ni mtaji na nyota muhimu inayotupa fursa ya kung’ara na kustawi kimaisha. Mathalani, zama hizi kipaji cha kusakata kandanda ni fursa na utajiri mkubwa endapo vijana wetu watuzitumia fursa zilizopo na sisi kuwapa fursa. Tusiwanyime fursa kama ambavyo Zanzibar imekosa fursa ya kung’arisha vijana wetu kusakata kandanda kimatiafa kupitia CAF barani Afrika na ulimwenguni kote kupitia FIFA. Vipaji vinatupa nafasi ya kugundua malengo muhimu katika maisha yetu na kutuwezesha kuyatimiza.

Nimesema kila mtu aliletwa hapa duniani kwa kusudi maalum na la kipekee. Ili kutekeleza kusudi hilo, Mungu katujaalia vipaji vya uimbaji, uigizaji, ufundi, uchoraji, uchongaji, ususi, uchezaji muziki, uchekeshaji, uchezaji michezo mbalimbali, ujasiriamali, utabibu, ualimu, uongozi katika jamii, ugunduzi, nk. Ni vipaji ambavyo tunazaliwa navyo kwa ajili ya faida ya mwenye kipaji na jamii nzima.

Nimebahatika kuzunguka nchi nzima na kuona vijana wanavyotengeneza simu kwa uhodari lakini hatuna shule au chuo chochote cha kufundisha kutengeneza simu. Ni vipaji vya ufundi wa vifaa vya elektroniki ndani ya vijana. Wanajitahidi sana kuvionesha vipaji vyao, lakini kwa bahati mbaya tunathamini sana vyeti badala ya ubunifu na vipaji. Tunapaswa kuvitambua, kuvienzi, kuviendeleza na kuwatunukia vijana hawa. Vitabu tunavyosoma, teknolojia tunayoiona, sanaa tunayoishuhudia, nk.; vilivumbuliwa na wenye vipaji maalum, wengine hata bila ya kwenda shule maalum au rasmi.

Najua kuna watu wanalalamikiwa au kulaumiwa kuwa hawana ubunifu. Lakini kila mtu ana upekee katika jamii kupitia kipaji chake. Hakuna mtu yeyote yule mwenye afya njema asiye na kipaji. Kuna mtu nyumbani kwetu Mwakaleli anapiga sana marimba na kuimba. Kila afikapo na kuanza kupiga na kuimba, watu huacha kazi zao na kujumuika naye kujimwayamwaya. Anapaswa kupewa fursa na kuanza kufaidika na kipaji chake huku akiendelea kutuburudisha kwa kipaji chake cha kuparaza marimba.

Hata hivyo, watu wengi tunashindwa kabisa kuvitambua, kuviendeleza na kuvitunza vipaji vyetu. Unaweza ukawa unatafuta mtaji wa kuanzia maisha au kuzunguka kila kona kutafuta ajira, kumbe unatembea na ajira au mtaji wako ambao labda ni sauti yako nzuri kwa kuimba. Ni muhimu sana kutambua kipaji chako ambacho ni mtaji wa kukupa ajira. Ukitambua kipaji chako na kukitumia ipasavyo utakuja kuwa mtu muhimu sana katika jamii.

Vijana wanaosakata kandanda, hasa nchini China na katika nchi za Ulaya, wana mishahara minono na mikubwa kupindukia ambayo hulipwa ndani ya juma moja. Hawasubiri mwisho wa mwezi. Kuna baadhi yao hulipwa takribani shilingi milioni 600 kwa juma! Ni kweli wengi hawajasoma lakini vipaji vyao vya kusakata kabumbu vimekuwa mtaji unaowafanya wawe matajiri kuliko wasomi na kuweza kuwaajiri wasomi.

Wengi tuliosoma na kuwa na shahada na utaalamu wa kutukuka, hatuufikii utajiri wa Nasib Abdul almaarufu Diamond Platinumz. Kipaji chake cha kuimba kimemfanya awe tajiri mkubwa na mwenye miradi ya maana. Aidha, nadhani wanaoongoza kwa utajiri duniani si wafanyabiashara, bali wale wanaotumia vipaji vyao kujiendeleza kama ambavyo Bill Gates hakusoma sana, lakini kipaji chake cha ufundi wa kompyuta na vifaa vya elektroniki, kimemfanya awe tajiri namba moja duniani kote.

Angalia mazingira unayoishi na watu wanaokuzunguka. Kama wanapenda kipaji chako na kukuunga mkono endelea kuishi hapohapo, lakini kama hakuna anayejali kipaji chako nenda sehemu unayokubalika. Kama unaishi sehemu ambayo hawathamini muziki wa ala na nyimbo zako za asili, tafuta mahali pengine na kuendeleza kipaji chako huko. Maisha ni kipaji chako na unaweza kuishi na kustawi nacho popote pale.

Ili kudumisha kipaji chako, nashauri kifanyie mazoezi na tunza mwili wako. Mazoezi huimarisha na hukomaza kipaji chako. Kuna haja kubwa ya kukifanya kipaji chako kionekane na/au king’are ili watu wakuone na kuutambua uwezo wako na kisha kukutambua wewe baada ya kwanza kujitambua wewe mwenyewe. Kipaji chako kikubebe na kukuinua badala ya kuwategemea wanadamu wanaoweza kukuingiza katika utumwa na kukunyonya. Kipaji chako awe ndiye mwajiri wako mkuu – boss wako!

Je, unapenda ufugaji? Fuga na jiendeleze. Je, unapenda kilimo? Lima na jiendeleze. Je, unasukumwa kufundisha katika fani fulani unayoipenda? Jifunze ualimu uwe mwalimu wetu. Je, una ufundi wowote? Ongeza maarifa na vifaa. Je, unaguswa kuitumikia jamii? Jitume na uwe na huruma, ukarimu, kujali wengine na moyo wa utumishi kwa wengine, maana hiyo ni misingi ya utu. Mojawapo ya hayo, ni kipaji chako ulichojaaliwa nacho.

Aidha, uwezo wako wa kuongea vizuri, kuimba vizuri, kuchekesha wengine, kupiga vizuri ala za muziki, kuumudu mchezo wowote ule ikiwemo kusakata kandanda, kusuka, kufinyanga vitu, kushona, kupamba sehemu mbalimbali, kupika vizuri, kutengeneza vitu mbalimbali, kuandika mambo mbalimbali, kuchonga vitu mbalimbali, kuchora picha mbalimbali, nk.; ni kipaji, kipawa, ajira na mtaji wako wa kukufanikisha kimaisha. Uwezo huo upalilie, uendeleze, uimarishe, utunze na jitunze ili uufaidi na kuwafaidisha wengine.

TANBIHI: Makala hii ya Gwappo Mwakatobe ilichapishwa kwa mara ya kwanza na gazeti la Mwelekeo la tarehe 1 Agosti 2017


Filed under: JAMII Tagged: ajira, kipaji, mafanikio, mtaji, uchumi Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Nguzo ya nne ya mitaji ya mafanikio ni rasilimali asilia

Hadi sasa, kwa msomaji anayefuatilia mfululizo wa uchambuzi wangu wa nguzo za mitaji halisi ya kutufanikisha katika maisha, atakuwa amegundua kuwa kumbe ni kweli kwamba fedha si mtaji, bali ni matokeo au mapato yatokanayo na mitaji mingine. Vitu vyenye thamani kubwa kuliko vyote si fedha, bali afya njema, fikra, vipaji ndani ya watu, na sasa rasilimali asilia.

Wanaoujua uchumi wa dunia hukiri kuwa akiba nzuri na njema si fedha zilizoko benki au mfukoni mwako. Yale ni makaratasi tu au namba, bali ukiweka akiba ya madini kama dhahabu, almasi na vito vingine vya thamani, na ukamiliki ardhi, una akiba isiyoyumba, isiyooza wala kuathiriwa na chochote, hata ukitokea mfumuko wa bei za vitu vyote. Thamani ya ardhi, madini na rasilimali zingine asilia, ndio utajiri wa uhakika duniani kote. Hivyo basi, katika makala haya nitazijadili rasilimali asilia zikiwa mojawapo ya nguzo za mitaji ya kustawisha maisha yetu.

Rasilimali asilia (natural resources) ni urithi mkubwa tulionao hapa duniani. Rasilimali (resources) ni vitu vyote vinavyotumika vinapohitajika. Hapa neno asilia (natural) ni kitu chochote cha asili, kinachopatikana katika mazingira yetu pasipo kutengenezwa, kuumbwa au kusindikwa na watu. Rasilimali asilia (natural resources) ni vitu vya asili kama vile hewa, maji, ardhi, vyanzo vya nishati (mfano mwanga wa jua, gesi asilia, makaa, mafuta ghafi, nk), mimea, wanyama, madini, anga, nguvu za uvutano (magnetic forces), nk.

Rasilimali asilia hutumika kukidhi mahitaji ya viumbe hai tukiwemo watu, maana nasi ni rasilimali watu (human resources). Dunia yetu ni sayari pekee iliyojaa rasilimali asilia kwa wingi kila upande wa mazingira yetu. Uhai na maisha yetu hutegemea moja kwa moja uwepo wa rasilimali asilia. Viumbe hai hatuwezi kuishi bila hewa, maji na mimea. Hatuwezi kujenga nyumba, kupata makazi na chakula pasipo ardhi. Hatuwezi kuendesha mitambo, magari, ndege na vyombo vingine vya moto pasipo mafuta, upepo na madini ya chuma. Pasipo jua hatuwezi kuwa na mimea, umemejua na mwanga.

Tayari nimejadili katika makala yaliyopita nguzo za mitaji ya mafanikio ya afya njema ya miili, fikra na vipaji. Lakini nguzo hizi haziwezi kufanya kazi pasipo rasilimali asilia. Kwa sasa dunia inakaribia kuwa na watu wapatao bilioni nane. Kadri watu tunavyoongezeka ndivyo mahitaji ya rasilimali asilia huzidi kuongezeka. Mahitaji ya watu yamekuwa mengi na shughuli zimezidi kuongezeka na kusababisha upungufu kwa baadhi ya rasilimali asilia. Niainishe kidogo baadhi ya rasilimali asilia muhimu kama ifuatavyo:

  • Hewa

Kama tujuavyo, hewa safi ni muhimu sana kwa ajili ya uhai wetu duniani. Na bahati iliyoje kwamba hewa hupatikana bure kwa ajili yetu, mimea na wanyama. Endapo hewa ingekuwa inauzwa kama tunavyouziwa mafuta, umeme, vyakula, nk.; naamini wengi tungepukutika! Kutokana na umuhimu huo wa hewa safi kuna haja ya kuongeza juhudi za kudhibiti uchafuzi wa hewa.

  • Maji

Japo dunia kwa sehemu kubwa imefunikwa na maji lakini mengi hayajahifadhiwa na kusambazwa vya kutosha ili kukidhi mahitaji ya nyumbani, viwandani na umwagiliaji. Tumewahi kujadili huko nyuma kuwa maji ni rasilimali asilia yenye upekee kwa kuwa haina mbadala.

Nchi yetu imebarikiwa sana kwa kuwa na rasilimali maji kwa wingi. Ni mtaji muhimu kwa maendeleo ikiwa tutaitunza, kuihifadhi na kuitumia vizuri. Misri ina mto mmoja tu, lakini inautunza na haijawahi kukumbwa na njaa au kukosa nishati itokanayo na maji. Sisi tuna mito mingi na vyanzo vingi vya maji pamoja na mvua nyingi lakini hatuitumii ipasavyo kwa ajili ya maendeleo yetu.

  • Vyanzo vya nishati

Vyanzo vya nishati ni kama mwanga wa jua, upepo, makaa, mafuta ghafi, gesi asilia, nk. Uhai wetu, mimea na wanyama hutegemea sana nishati ya jua. Upepo tunautumia kujaza matairi ya magari na kuzalisha umeme. Makaa ya mawe yanatumika sana viwanadani na nyumbani. Mafuta, iwe dizeli, petroli, gesi asilia au mafuta mazito, huendesha mitambo na kuturahisishia kufanyia kazi mbalimbali.

Kuna nchi ambazo ni tajiri sana kutokana na rasilimali ya mafuta, hasa nchi za Uarabuni, Amerika Kusini na baadhi ya nchi za Afrika. Miaka ya hivi karibuni Tanzania pia imegundua kiwango kikubwa cha mafuta na gesi asilia hususan ukanda wa mwambao wa Pwani na maeneo ya bonde la ufa. Dunia nzima inasadikika kuwa na akiba ya mafuta na gesi asilia ardhini ya kututosha kwa miaka 60 hadi 100.

  • Ardhi

Ardhi ni rasilimali muhimu sana na wakati huohuo ni mtaji mkubwa kote duniani. Haijawahi kupungua thamani hata siku moja! Kila tunachokula hutokea ardhini. Ukila mboga, kunde, matunda, wanga, nyama, nk.; hutokana na ardhi. Mwili huu hulishwa na vitu vinavyotoka ardhini. Mboga humea kwa kunyonya virutubisho vya kwenye udongo na kisha kuingia na kuijenga miili yetu.

Nyama tunazokula pia hutokana na udongo pale ambapo wanyama hula nyasi, zikajenga nyama zao na kisha kuja kwenye miili yetu tunapokula. Tuna miili ya udongo na kwenye udongo inarudi. Aidha, ardhi ni hifadhi kubwa ya rasilimali zingine kama madini (dhahabu, almasi, chuma, nk.), mafuta, gesi, makaa na maji.

  • Madini

Utajiri wa madini na umuhimu wake tunaujua. Ni hivi karibuni tulisikia makampuni mbalimbali duniani yanavyotajirika kwa uchimbaji wa madini hasa yaliyopo barani Afrika. Tanzania tumebarikiwa kuwa na aina nyingi za madini ambapo hatuwezi kutembea kilomita 5 bila kuwepo kwa aina fulani ya madini.

Kuna haja ya kuungana pamoja kuhakikisha kuwa rasilimali madini inanufaisha vizazi vilivyopo na vijavyo pasipo kuruhusu uporaji unaoendelea sasa. Na kwa kusema hivyo, tuiombee na kuisimamia serikali iweke mbele uzalendo katika mikataba. Pale itakapobidi makampuni yanayotupora yasitishwe kwa kuwa hata tusipochimba sasa madini hayataoza, watakuja kuchimba watoto wa watoto wetu.

  • Mimea

Tuna kila aina ya mimea. Tuna misitu, vichaka, nyasi, nk. Mimea inatupa mboga, mbegu za vyakula mbalimbali, dawa za kila aina na miti ya kujengea nyumba zetu na kutoa samani za kila sampuli. Tusisahau pia kuwa hewa safi tunayovuta ya oksijeni inatokana na mimea. Hewa chafu ya ukaa tunayoitoa humezwa na mimea. Mimea kama mchicha, pilipili, bamia matikiti, miti ya matunda, nk.; ni nguzo muhimu ya mitaji ya mafanikio katika uhai na maisha yetu.

Ukiwa na kipande cha ardhi, ukiwa na msitu, ukiwa na kisima cha maji, una utajiri mkubwa wa kukupatia chochote utakacho. Si rahisi kuibiwa au kushuka thamani. Gari linachakaa na kuharibika, fedha taslimu unaweza kuibiwa au zikashuka thamani, lakini si ardhi. Nawaasa Watanzania wote tutawanyike kwenda kwenye maeneo ya wazi tukashike na kumiliki ardhi, kabla ya sisi na watoto wetu hatujawa wapangaji katika ardhi ya nchi yetu!

TANBIHI: Makala hii iliyoandikwa na Gwappo Mwakatobe ilichapishwa kwa mara ya kwanza na gazeti la Mwelekeo la tarehe 7 Agosti 2017.


Filed under: JAMII Tagged: ardhi, bahari, maji, mimea, mtaji, rasilimali, uchumi Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Ndani ya mwani, muna fursa kubwa ikiwa Zanzibar itajipanga

Licha ya Zanzibar kutajwa kuwa nchi ya tatu duniani kwa kuzalisha mwani kwa wingi na wenye kiwango kizuri, bado wakulima wanalalamika kutofaidika vya kutosha kwa kilimo hicho.

Wakulima wa mwani ambao ni zaidi ya 20,000 visiwani Zanzibar – wengi wao wakiwa wanawake wa vijijini – wamekuwa wakipanza sauti zao kutokana na bei ndogo, kodi iliyokithiri, ukosefu wa vifaa na kufanyakazi katika mazingira magumu.

Kuelekea uchaguzi mkuu wa 2015, wanasiasa wa pande zote mbili kuu waliyatumia sana majukwaa ya kampeni kwa kuwaahidi wakulima wa zao hilo  kwamba wangeliwabadilishia maisha yao kwa kuimarisha kilimo hicho.

Dk. Ali Mohamed Shein wa Chama cha Mapinduzi (CCM) aliahidi ugawaji wa vihori (vifaa maalumu vya kubebea mwani baada ya kuvunwa baharini) na pia kujenga viwanda vya usindikaji zao hilo hapa hapa Zanzibar.

Lakini hadi leo, wakulima na wauzaji wa mwani wana kilio kile kile cha awali – kodi iko juu, bei ni ndogo, gharama za kilimo haziendani na mapato.

Katika maonesho ya Siku ya Mwani Zanzibar mwaka huu, mkulima Mariam Pandu Kweleza kutoka kijiji cha Bwejuu alimuambia mkuu wa shughuli za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), Balozi Seif Ali Idd, kuwa kazi wanayofanya ni ngumu  na huku pato wanalolipata si robo ya maumivu ukulima wa kilimo hicho.

Image may be NSFW.
Clik here to view.

Baadhi ya bidhaa zitokanazo na mwani wa Zanzibar.

“Mheshimiwa, kilo twauza kwa shilingi 300. Kweli zitaweza kufuta jasho letu? Kazi hii ni ngumu mno na sasa hivi tunaambiwa ni zao la tatu kwa kuingiza fedha za kigeni lakini wakulima bado twaumia!”

Alieleza kuwa bei ya zao hilo inapangwa na makampuni bila kuangalia kazi ngumu zinazofanywa na wakulima hao, ambao wengi wao ni wanawake tena wajane.

Amina Khamis, muuzaji wa bidhaa zinazotokana na zao la mwani, anasema kuwa makato wanayokatwa ni makubwa kupitia taasisi mbili tofauti zza kodi – Mamlaka ya Mapato ya Tanzania (TRA) na Bodi ya Mapato ya Zanzibar (ZRB), ambapo muuzaji mwani nje ya Tanzania hukatwa asimilia mbili ya kodi ya ongezeko la thamani (VAT) utoka TRA na baada ya mauzo hayo hukatwa tena asimilia kutoka ZRB.

Kilio cha wakulima na wafanyabiashara ya mwani kinafanana na sekta nyengine zote za biashara zinazofanyika Zanzibar. Mapungufu ni yale yale, madai ni yale yale, ahadi ni zile zile, lakini kisha hali inasalia kuwa vile vile.

Je, kuna jitihada zozote za kubadilisha mambo? Ndiyo, katika kutafuta njia ya kuwanyanyua na  kuwaendeeleza wakulima hao ambao hufanya kazi zao baharini, Taasisi ya Milele Zanzibar Foundation imekuja na mpango maalumu kwa kushirikiana na Taasisi ya Zanzibar Seaweed Cluster Initiative ( ZaSCI) kuongeza usarifu na matumizi ya mwani na kupandisha juu mahitaji na matokeo yake, kwa hivyo, kupandisha bei ya zao hilo.

Bi Khadija Shariff, Mkurugenzi Mtendaji wa taasis ya Milele Zanzibar Foundation, anasema ili kufikia hatua hiyo panahitajika kwanza kuwa “viwanda vya kusarifia mwani ndani ya nchi ambapo ndani yake utaweza kutengeneza sabuni za mwani, shampoo, dawa za meno, poda, mafuta ya kung’arisha mwili, keki, jam…”

“Ikiwa ushirikiano nzuri baina ya wazalishaji na taasisi utaendelea, basi hakuna litakaloshindikana”, anaongeza Bi Khadija.

Image may be NSFW.
Clik here to view.

Mwani wa Zanzibar unaweza kuwa njia kuu ya uchumi wa visiwa hivi vidogo lau nchi itajpanga kikamilifu.

Milele Zanzibar Foundation inajihusisha, pamoja na mengine, na kutafuta fursa zilizopo visiwani Zanzibar hasa zile zinazoweza kuwainua kiuchumi wananchi wa visiwa hivi. Ndipo ilipogundua kuwa zao la mwani linaweza kuwa ni miongoni mwa fursa kuu zinazopatikana na zinazoweza kuwakwamua kiuchumi wakaazi wa visiwa hivi vya Bahari ya Hindi.

Baada kutambua na kuvutiwa na kazi nzuri za Kongamano Bunifu la Mwani Zanzibar mwaka 2015, taasisi hiyo sasa imeungana mkono na kongamano hilo ili kuwajengea uwezo wakulima na wasarifu wa mwani katika kupata taaluma na kuwawezesha katika kujenga mashirikiano mazuri na wadau wengine wa sekta ya mwani.

“Hadi sasa tumeweza kufanikisha uzinduzi wa Siku ya Mwani Zanzibar kwa lengo la kuutangaza na kueneza uelewa wa matumizi na faida za mwani,” anaeleza Khadija.

“Tunaishukuru Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kwa kuamua kuwa siku hii itakuwa inaadhimishwa kitaifa kila mwaka.”

Alieleza kuwa wamefanikiwa kuwapatia wakulima na wasarifu wa mwani elimu ya ujasiriamali na kuwafumbua macho namna ambavyo wanaweza kujikomboa kimaisha kupitia zao hili.

“Pia tumefanikiwa kuwakutanisha wakulima, wasarifu, wauzaji, wasafirishaji na wadau wote wa mwani  kwa kufanya mikutano kila baada ya miezi mitatu kwa lengo la kujadili changamoto zinazoukabili mwani na namna ambavyo wanaweza kujinasua katika changamoto hizo,” anafafanua Khadija.

Mwani huuzwa na kutumiwa sana katika mataifa ya  Japan, China, Korea Kusini, Denmark, Ufaransa, Singapore na Marekani kama chakula na bidhaa nyengine.

Kwa Zanzibar, biashara ya zao hili ilikuwepo tangu miaka ya 1950 kwa kuokotwa mwani wa asili baharini, lakini kuanzia mwaka 1989 ukaanza kulimwa rasmi kwa mbegu za kutoka Ufilipino. Mbegu hizo aina ya Spinosum na Cottonii ndizo zinazolimwa hadi hivi leo.

TANBIHI: Makala hii imeandikwa na Talib Ussi


Filed under: JAMII Tagged: milele foundation, mwani, uchumi, Zanzibar Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Maalim Seif, Profesa Lipumba ndio pekee wa kuinusuru CUF

Binafsi sioni ushindi kwa yeyote kati ya Profesa Ibrahim Lipumba na Maalim Seif Sharif Hamad katika mgogoro unaoendelea sasa kwenye Chama cha Wananchi (CUF), bali ushindi pekee ni kwa wawili hao kupatana, kusameheana na kukiunganisha chama na wanachama.

Najua ni ngumu na yataka moyo, lakini wakati wote ukifaulu kufanya mambo magumu kwa kuthubutu na kujituma, mwishowe ushindi wake ni mtamu na hudumu.

Lipumba na Seif wametoka mbali na kufanya pamoja mambo mazuri mengi yanayowaunganisha zaidi kuliko mabaya machache yanayowatenganisha, huku wakiongoza chama ambacho kina historia ya mafanikio makubwa kwenye kuimaliza migogoro ya mazungumzo.

CUF waliwahi kuitwa na CHADEMA CCM B, lakini sasa vyama hivyo viwili ni marafiki wa chanda na pete kwenye muungano wao wanaouita UKAWA, Umoja wa Katiba ya Wananchi.

Dunia pia imejaa mifano tele ya aina hii. Nelson Mandela, mathalani, aliwahi kuteswa na makaburu lakini alipopata urais alifanya kazi nao pamoja na kuunda tume ya ukweli, maridhiano na kusameheana. Mandela alimpa mpinzani wake Chifu Mangisuthu Buthelezi wizara nyeti.

Raila Odinga nchini Kenya alihasimiana sana kisiasa na Mwai Kibaki na ukatokea umwagaji damu mkubwa. Baadaye walipatana wakawa pamoja, Raila Odinga akiwa Waziri Mkuu na Mwai Kibaki akabakia Rais.

Je, nani alitegemea uhasama na shutuma alizopata Lowassa, hasa kutoka CHADEMA kwa takribani miaka 8, leo hii angekuwa kada tegemeo kwa CHADEMA?

Mwaka 2000 Maalim Seif alipokosa urais dhidi ya Amani Abeid Karume yaliibuka machafuko makubwa yaliyomwaga damu nyingi Januari 2001 na kuzalisha wakimbizi. Lakini baadaye alipatana na Karume mpaka ikarekebishwa katiba iliyozaa serikali ya umoja wa kitaifa mwaka 2010.

Kumbe kwa upande mwingine, Maalim Seif ni mvumilivu, msikivu na mpenda majadiliano na upatanishi. Kama Maalim Seif alipatana na kufanya kazi pamoja na wana CCM kwa miaka mitano akiwa Makamu wa Kwanza wa Rais, sioni kama atashindwa kupatana na Lipumba aliyefanya kazi naye kwa muda mrefu akiwa Mwenyekiti wake.

Ndani ya CUF, si mara ya kwanza kwa Maalim Seif kukosana na viongozi wenzake, wakiwemo James Mapalala na Hamad Rashid Mohammed. Bahati mbaya hakuwahi kusuluhishana na kupatana nao.

Sasa ni fursa adimu na adhimu kwake kukutana, kusalimiana na kusuluhishana na Lipumba. Chonde chonde Profesa Lipumba na Maalim Seif nawaomba tulieni, tafakari na kaa pamoja. Kumbukeni mema mengi mliyofanya pamoja na muyaenzi kwa kufuta mabaya machache yaliyojitokeza ili mpate ushindi pekee na utakaowaletea heshima kwa Watanzania na kukiunganisha chama na wanachama wenu.

Maelewano, mapatano na maridhiano ni mbegu njema kwa watoto na watoto wa watoto wetu kama alivyofanya Mandela.

Napendekeza jamii ya wapenda amani, demokrasia na upatanishi, tuwawezeshe Profesa Ibrahim Lipumba na Maalim Seif kukutana ana kwa ana, na kila mmoja apewe nafasi ya kusikilizwa vya kutosha kwa kile kinachomuumiza na kumsumbua dhidi ya mwenzake.

Kisha pale inapowezekana, kila mmoja aeleze yale ambayo anaona mwenzake amewahi kufanya vizuri au kila mmoja ataje mema ambayo anaona mwenzake anayo. Mimi binafsi, ikiwapendeza wahusika, najitolea kuwapatanisha viongozi hawa. Najua sina cheo au wadhifa wowote mkubwa katika jamii, lakini najisikia uchungu na maumivu yaleyale wanayoyapata hawa wawili, wanachama wa CUF na wote wanaopenda amani.

Kwa yeyote mwenye mawasilino na hawa wawili aniunganishe nao. Vyama vya upinzani hususan vya muungano wa UKAWA, kama wataitambua busara hii, watoe tamko la kuunga mkono upatanishi huu.

Tuwaponye wanachama na kuwaonesha ukomavu wetu wa kutatua migogoro. Ndio njia pekee na bora kabisa ya kumwaibisha adui anayeutumia mgogoro huu kudhoofisha vyama vya siasa na demokrasia nchini.

Profesa Lipumba na Maalim Seif wakubali kustaafu na kubakia wazee wastaafu wa chama wenye busara. Sambamba na hilo, katiba ya chama irekebishwe ili kuweka kipengele maalum cha baraza la busara na ushauri la wazee wastaafu. Na kisha uchaguzi maalum ufanyike ili kujaza nafasi ya Mwenyekiti na Katibu Mkuu Taifa.

Mwishowe, iandaliwe hafla fupi na chakula maalum cha kuwakutanisha, kuwapongeza, kuwaenzi na kuwaaga rasmi wastaafu Profesa Ibrahim Lipumba na Maalim Seif. Kwenye hafla hiyo waalikwe viongozi wa vyama vyote vya siasa, viongozi wa kijamii na watu maarufu wenye hekima kutoka ndani na nje ya nchi. Washuhudie na kutoa nasaha zao za jinsi Waafrika tunavyotatua migogoro yetu kwa ustaarabu na uungwana wa Kiafrika.

Nihitimishe kuwa kabla ya kufariki Januari 30 1948, Mohandis Karamchand Ghandi, almaarufu Mahatma Ghandi, alituasa kwa kusema, nanukuu: “Kazi yangu katika maisha kwa miaka 33 iliyopita, imekuwa kuorodhesha urafiki na watu wote, kwa kuwafanya wawe marafiki bila kujali asili ya mtu, rangi au imani.”

Naam, Lipumba na Maalim Seif rejesheni urafiki wenu, na mnayo nafasi na ushawishi mkubwa wa kukinusuru chama.

TANBIHI: Makala hii imeandikwa na Gwappo Mwakatobe, mwandishi na mchambuzi wa masuala ya kisiasa na kijamii anayeishi Mwakaleli, Mbeya, kama sehemu yake ya kuchangia suluhu ndani ya CUF. Mwandishi anapatikana kwa anwani za barua-pepe gwandumi@hotmail.com na au gwappomwakatobe@gmail.com


Filed under: SIASA Tagged: cuf, maalim seif, Profesa Lipumba, Tanzania Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Ya uchaguzi Zanzibar nayo dhambi

MOJA ya kauli nzito ambazo Rais Dk. John Magufuli amekuwa akizitoa wakati huu anapoendelea kuzunguka nchi kwa ziara rasmi ya kiserikali anayoiita ni ya kushukuru wananchi kwa kumchagua kuongoza Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ni kushughulikia au kufuta dhambi.

Rais Magufuli anasema anafuatilia dhambi dhidi ya Taifa na Watanzania. Ni dhambi zilizopita. Ni dhambi zilizotokana na awamu zilizopita za uongozi wa nchi. Awamu za uongozi zenyewe zote zimekuwa chini ya Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Chama hicho kilichukua uongozi kama mrithi wa vyama vya Tanu na Afro-Shirazi (ASP), vilivyopigania uhuru wa Tanganyika na Zanzibar, nchi zilizozaa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania baada ya kuunganishwa tarehe 26 Aprili 1964. CCM ilizaliwa tarehe 5 Februari 1977 kufuatia kuunganishwa Tanu na ASP.

Rais Magufuli, kama walivyo marais waliomtangulia, ameingia uongozini kupitia chama hicho CCM; leo anaomba wananchi ambao anajivuna kuwa ndio waliompa ridhaa ya kuongoza, wamuunge mkono kwa namna mbalimbali katika kushughulikia dhambi.

Anasema anatenda kwa kuwa anawapenda wananchi na anasema anausema ukweli huo kwa kuwa msema kweli ni mpenzi wa Mungu. Kama hiyo haitoshi, anasisitiza kwamba yeye ni rais wa wananchi wote na kwa hivyo anavyoenenda, anafanyakazi hiyo katika kuwatumikia Watanzania wote. Wao wananchi basi, wanao wajibu wa kuonesha moyo na kumuombea kwa Mwenyeezi Mungu.

Rais anasema anashughulikia mambo hayo ambayo yalifanywa kifisadi na kwa ajili ya maslahi binafsi ya wahusika hao na familia zao, matokeo yake yakawa ni kuwaumiza wananchi kwa kuwa yamesababisha serikali kunyimwa uwezo wa kuwahudumia kwa ufanisi.

Maelezo yake yana maana kuwa kwa kutendwa mambo ndivyo sivyo yanayohusu uendeshaji wa serikali ukitumia raslimali zake, watendaji wa serikalini na washirika wao waliofadhili mipango ya kutafuna au kufisidi uchumi wa taifa, walisababisha serikali ikose mapato stahili lakini pia waliifedhehesha serikali na kwa upana wake, jamhuri.

Katika lugha ya picha, mara nyingi ukiitafsiri unapata nguvu ya kuamini kuwa ni kweli huyu rais wa awamu ya tano, anakusudia kusema kazi hiyo anayoifanya ni jambo jema na katika kutimiza dhamira aliyoahidi wakati wa kampeni ya uchaguzi, ya kuwatumikia Watanzania wa vyama vyote vya siasa na hata wasiokuwa na vyama, hatofanya ubaguzi wa aina yoyote.

Wananchi wa Tanzania au Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wamekuwa wakishuhudia utendaji serikalini ukileta matokeo yanayoathiri maisha yao ya kila siku. Matendo yanayofanywa na watumishi waliopewa dhamana na serikali ya wananchi yamekuwa mabaya na yakisababisha dhulma kubwa dhidi yao kwa muda mrefu.

Tayari katika utekelezaji wa dhamira yake rais, kuna idadi si haba ya kesi zimefunguliwa kwenye mahakama zetu na nyingi zingali katika hatua ya upelelezi.

Kwangu binafsi leo, nataka kuweka kumbukumbu vizuri kwamba nimekuwa napata uzito kumuelewa rais. Kwamba ni kweli amekusudia kufuta dhambi walizotendewa wananchi? Ni kweli anafuta dhambi kwa yote mabaya yaliyofanywa au anachagua baadhi yao huku mengine akiwa anayapita?

Je, utekelezaji wake wa kufuta dhambi unayaangalia hayo mabaya kwa kigezo cha uzito au anachukua hili na jingine kuliwacha? Isitoshe, anapofuta dhambi kwa yale maovu yaliyofanywa huko nyuma, analenga kuinua taswira ya nchi na watu wake kama nchi inayojali haki za watu au anakipalilia tu chama kilichompa ridhaa ya kuwania uongozi wa juu nchini? Niliseme moja. Suala la Zanzibar.

Kwamba Rais Dk. Magufuli ameridhika na msimamo wake ambao ndio msimamo khasa wa CCM kuwa Zanzibar isubiri uchaguzi mkuu wa mwaka 2020? Kwamba huo bado ni msimamo anaouamini kuwa unastahili?

Inawezekana Rais amesahau ahadi yake alipohutubia Bunge jipya la 11 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, siku ambayo alikuwa analizindua tarehe 20 Novemba 2015.

Pale aliposema kuwa Zanzibar kuna tatizo kidogo katika uchaguzi wao na akaahidi kuwa atalitafutia ufumbuzi kwa kushirikiana na makamu wake, Mama Samia Suluhu Hassan, pamoja na Dk. Ali Mohamed Shein, alilenga kitu gani hasa?

Nataka kuamini kuwa alilijua kwa upana wake tatizo alolitolea ahadi kulitafutia ufumbuzi. Niamini alijua hivyo, kwa sababu zinajulikana njia kadha wa kadha za kuelezwa kilichotokea kuuhusu uchaguzi mkuu wa Zanzibar uliofanyika siku ileile ya tarehe 25 Oktoba 2015, ya uchaguzi mkuu kwa upande wa nafasi ya rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wabunge na madiwani wa Bara.

Kama Rais Dk. Magufuli alijua tatizo lililopo ndipo akathubutu kujitwika jukumu la kulimaliza ili Jamhuri yote iwe na amani na salama, miaka miwili sasa ikikaribia tangu pale, ndo tuseme ameridhika kabisa kuwa ameitimiza ahadi yake?

Ule msimamo mpya na mkali alioutoa wakati alipofanya ziara ya mikutano miwili Zanzibar – wa kwanza ukiwa uliofanyika kwenye Uwanja wa Gombani ya Kale, mjini Chake Chake, Pemba, na wa pili uliofanyikia Uwanja wa Demokrasia Kibandamaiti mjini Unguja – kwamba Dk. Shein ndiye rais aliyechaguliwa na wananchi wa Zanzibar, anaushikilia hata leo?

Siamini. Rais alitoa msimamo wa haki akiwa mbele ya Bunge siku ile Novemba 2015. Aliaminika kuwa amemaanisha au kama Waswahili wapendavyo kusema, “atatembea kwa maneno yake.” Ila kwa msimamo mpya kwenye majukwaa ya CCM ameondoka alipoahidi, na kuamua kupuuza au kuikanyaga ahadi yake.

Hivi Zanzibar ilivyo sasa imegawanyika huku zaidi ya nusu ya watu wakiwa wanyonge kwa sababu ya kuamini hawajatendewa haki kwenye uchaguzi ule, rais haoni kuwa anaongoza Jamhuri inayosononeka? Haoni kuwa ule umoja wa kitaifa na mshikamano wa kiuananchi uliokuwepo kabla na wakati uchaguzi unafanyika, umetikiswa na kutikisika vilivyo?

Ninamsihi atambue ukweli kuwa Zanzibar ambayo ni sehemu ya jamhuri anayoongoza tena akiwa ndiye amiri jeshi mkuu wa majeshi yote ya ulinzi na usalama; imegawanyika. Ni mgawanyiko uliotengenezwa kukidhi maslahi ya kisiasa zaidi kuliko kuona sehemu hiyo inapiga hatua ya maendeleo. Ni dhambi tupu ambayo mimi ninaamini asipoona hivyo leo, itakuja siku ataona, maana maji hayageuki maziwa hata yakipakwa rangi vipi.

TANBIHI: Makala hii ilichapishwa kwa mara ya kwanza na gazeti la MwanaHalisi la tarehe 7 Agosti 2017.


Filed under: HABARI Tagged: jecha, Magufuli, Zanzibar, ZEC Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Nguzo ya tano ya mitaji ya mafanikio ni maarifa na elimu

“Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa…” (Hosea 4:6), ndivyo Mungu anavyosikitika na kutoa sababu ya watu wetu kuangamizwa kuwa ni ukosefu wa maarifa. Tunalalamika kuwa tu maskini, lakini hapohapo tena tunajidai kuwa tuna utajiri wa rasilimali asilia nyingi na za kututosha. Umaskini unatoka wapi kama tuna utajiri huo wa rasilimali asilia lukuki?

Rasilimali asilia zikibaki zilivyo katika uasili wake, pasipo kuchakatwa, kuchenjuliwa, kusindikwa na kuboreshwa; haziwezi kutuletea mapato, faida na/au mafanikio. Lazima tupate maarifa na elimu (si wawekezaji uchwara) ya kuchakata, kuchenjua na kusindika rasilimali zetu ili kuziongezea thamani na kuziuza kwa faida katika masoko ya  kitaifa na kimatiafa.

Zanzibar ina utajiri mkubwa wa mwani, na ni mojawapo ya maeneo machache yanayozalisha mwani kwa wingi duniani. Lakini Wazanzibari wengi bado maskini. Tatizo liko wap? Tatizo ni kukosa maarifa, elimu na vifaa (teknolojia) stahiki ya kuuchakata, kuusindika, kuuboresha na kuuongezea thamani mwani kwa kuzalisha bidhaa zake mbalimbali kama wafanyavo wenzetu Singapore na Ufilipino. Tunahitaji maarifa ili tusizidi kuangamizwa na ufukara katikati ya utajiri wa mwani na rasilimali zingine.

Umuhimu wa Maarifa na Elimu kwa Maendeleo ya Watu

Maarifa ni ujuzi, umahiri, ufundi, ustadi au uhodari katika fani au nyanja fulani, ambayo kwa sehemu kubwa hutokana na kipaji alichonacho mtu na kukiboresha kwa elimu au utaalamu wa ziada katika fani husika. Maarifa na elimu ni msasa wa vipaji, na ni muhimu zaidi kuliko hata rasilimali asilia nilizozijadili makala ya nyuma. Kosa kila kitu, lakini si maarifa na elimu!

Leo hii nchi nyingi duniani hazina madini, misitu, wanyama, mafuta wala ardhi nzuri kwa kilimo; ila zina maarifa na elimu inayoziletea utajiri mkubwa. Mathalani Ulaya, nchi za Japan, Singapore, Korea Kusini, nk.; hazina neema ya rasilimali asilia kama tulizojaaliwa Afrika, hususan kusini mwa jangwa la Sahara, lakini matajiri. Watu wake wanafaidi rasilimali zetu kuliko sisi wenye nazo. Wanatuzidi nini sasa? Maarifa na elimu!

Mkamate sana elimu, usimwache aende zake; mshike, maana yeye ni uzima wako. Ndivyo tunavyoisoma hekima ya Mungu katika misahafu (Mithali 4:13). Kinara wa ukombozi wa utu wa mtu, hususan kwa Waafrika, Nelson Mandela, aliwahi kusema, ninanukuu: “Elimu ni silaha yenye nguvu sana ambayo unaweza kuitumia kuleta mabadiliko ulimwenguni.”

Neno elimu tumelitafsiri kutokana na neno la Kiingereza la “Education.” Education hutokana na neno la Kilatini la “Educare.” Educare means to draw out or to impart and fill. Yaani kwa tafsiri rahisi, “Educare” ni kuwa mpana zaidi/kutanuka au kuweka na kujaza. Tunapoelimishwa tunapewa uelewa mpana au kuwekewa na kujaziwa maarifa yanayotupa ufahamu, ustadi na ujuzi katika vichwa vyetu. Elimu si tu kujua kusoma na kuandika, la hasha; bali ni kuwa na maarifa, ujuzi, umahiri ua uhodari katika kukabiliana na changamoto za mazingira yetu na maisha yetu.

Elimu ni maarifa anayopata au anayokuwa nayo mtu ili aweze kuishi kwa kupambana au kuyamudu mazingira yaliyopo kupitia kipaji au utaalamu wake. Aidha, elimu huchonga, hupalilia, huchochea, huimarisha na huboresha kipaji cha mtu – inamfanya mtu awe na ufanisi. Bila elimu mtu huonekana hafai hata kama ana kipaji kizuri. Mtu asiye na elimu au mwenye kiwango duni cha elimu hujiona mnyonge na hukosa fursa nyingi za kujiendeleza kimaisha – anaangamizwa na ukosefu wa maarifa.

Tokea enzi na enzi elimu iliyorasmi na isiyorasmi hutafutwa popote pale na kugharimiwa ili kumtoa mtu katika ujinga na ufukara wa fikra. Kabla ya kuwa na shule na vyuo, watoto na vijana wetu walifundishwa na wazazi wao au jamii yao namna ya kuwinda, kurina asali, kuwasha moto kwa vipande vya miti na kuvipekecha kwa fimbo, kuvua samaki, kufuma nguo, kulima, kufua chuma, nk. Maarifa na elimu vilitolewa kwa njia isiyorasmi lakini iliyo thabiti, na tunaendelea kujifunza vitu vingi kwa njia zisizorasmi na rasmi. Vitabu, na sasa simu na kompyuta, ni hazina kubwa ya maarifa na elimu.

Elimu ipo katika nyanja mbalimbali na imekuwa ikiboreshwa kuendana na wakati kadri ugunduzi wa teknolojia na maarifa unavyozidi kuongezeka. Miongoni mwa walimu na wakufunzi wa elimu ni wazazi na/au walezi katika familia wakitufundisha masuala mbalimbali yahusuyo maisha yetu na mazingira yetu. Heshima na shukrani ziende kwa wazazi na walimu wote.

Elimu ina faida nyingi na muhimu sana katika maisha ya binaduamu. Mtu mwenye maarifa na elimu ana mtaji kwa ajili yake mwenyewe na pia naye ni mtaji kwa jamii na taifa kwa ujumla. Ndio maana serikali, taasisi na watu binafsi huajiri watu kulingana na viwango vyao vya maarifa, ujuzi na elimu.

Ulimwenguni kote rasilimali watu ni kwa watu wenye elimu na huchukuliwa kwa umuhimu wa pekee. Ingawa kila mtu ni muhimu katika jamii, na ana mchango wake – hata kama ni kubeba mizigo sokoni, lakini kwa dunia ya sasa thamani ya mtu imewekwa zaidi kwenye maarifa na elimu yake. Mtu mwenye maarifa na elimu bora hutafuta njia bora na vifaa au teknolojia stahiki ili kufanya kazi zenye tija, ufanisi na maendeleo.

Kadri tunavyoelimika ndivyo hata vipato vya maisha yetu huongezeka. Elimu pia hutuwezesha kuwasaidia wengine wasiokuwa na uelewa. Kwa muhtasari, baadhi ya manufaa na faida za elimu ni hizi zifuatazo:

  • Inatufanya tujitegemee na kuwa huru katika kufanya maamuzi sahihi na kwa weledi ili kujipatia kipato cha kuendeshea maisha yetu binafsi pasipo kumtumainia moja kwa moja mtu mwingine
  • Inatusaidia sana katika kuleta heshima ya kiwango fulani, sifa stahiki na usawa miongoni mwa wanajamii
  • Inatufanya tujiamini katika kujieleza na kutoa maoni, na watu hutuamini kutokana na kuthamini viwango vyetu vya elimu
  • Inatusaidia sana kupunguza kwa kiasi kikubwa umaskini uliokithiri miongoni mwa wanajamii na kutusaidia kuajiriwa na/au kujiajiri
  • Inatusaidia kuongeza tija katika uzalishaji mali na bidhaa mbalimbali kwa viwango vya juu
  • Inatusiaidia kustaarabika na kuishi maisha ya utengamano, uelewano na maridhiano miongoni mwa wanajamii na mataifa
  • Ni silaha kubwa ya kutokomeza ujinga na magonjwa, na aghalabu jamii huwa na mwamko mkubwa wa kutatua matatizo ya kiafya
  • Inatupa mwanga unaotuonesha jinsi ya kukabiliana na changamoto mbalimbali za kimaisha kwa ustadi na urahisi zaidi
  • Inatupa mbinu na njia mbalimbali za kuzibadili rasilimali asilia kuwa na tija na zenye faida katika maisha yetu
  • Taifa lenye watu walioelimika linakuwa na ukuaji wa kiuchumi (economic growth) na maendeleo ya kiuchumi (economic development).

Hitimisho

Urithi mkubwa na unaojitosheleza kwa watoto wetu si kuwapatia fedha, nyumba, ardhi, magari au vitu vyovyote vile tunavyomiliki. Bali ni kuwapatia maarifa na elimu. Ukimwezesha mtoto kusoma na kupata elimu, tayari umemrithisha na kumpa kila kitu. Unakuwa umemlipia mahari au umemwoza, umemjengea nyumba, umempa gari, umempa ajira na umempa mtaji wa kumsaidia yeye na familia yake. Unakuwa umempa utajiri, huna haja ya kuhangaika kumtafutia ajira au kuanza kumgawia mali yako kama urithi – urithi wake kutoka kwako unakuwa elimu na maarifa aliyopata.

Tukishapata maarifa na elimu, hatuwezi kuuza magogo ya miti au mbao zake, na kisha kununua kwa bei kubwa samani za thamani za miti na mbao hizohizo. Tukiwa na maarifa na kuelimika, hatuwezi kuuza ngozi za ng’ombe Kenya na kuja kununua viatu vya bei kubwa kuliko ngozi zetu tulizowauzia. Tukiwa na maarifa hatuwezi kuomba misaada kwa nchi zilizoendelea, bali tutachota maarifa na elimu ya nchi hizo ili ije itusaidie nyumbani.

Naam, tukiwa na maarifa hatuwezi kuuza makinikia huku tukiachiwa mahandaki na uharibifu mkubwa wa mazingira yetu. Bali tutahakikisha tunachenjua makinikia yenyewe sisi wenyewe na kuuza madini safi. Nchi za Japan, Malaysia, Singapore, Korea Kusini, Uswisi, nk.; zimeendelea baada ya kuchota maarifa na elimu ya kutosha na kuitumia nyumbani kwao.

Haziombi misaada au wataalamu wawaletee maendeleo. Hapana! Zinasaka maarifa na elimu ya kujiletea maendeleo yao. Tuyatafute maarifa na elimu popote duniani ili tusiendelee kuangamizwa na ujinga wetu. Maarifa na elimu ni nguzo ya mitaji ya kutuletea mafanikio katika maisha yetu. Tukibaki na ujinga wetu tunakuwa katika hatari ya kunyonywa na kutumika au kutumiwa na wengine kwa faida yao.

TANBIHI: Makala hii imeandikwa na Gwandumi Gwappo A. Mwakatobe, mchambuzi huru wa masuala ya kitaifa na kimataifa, anayeishi Mwakaleli mkoani Mbeya. Anapatikana kwa anwani ya baruapepe: gwandumi@hotmail.com au gwappomwakatobe@gmail.com


Filed under: JAMII Tagged: elimu, maarifa, mafanikio, uchumi Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

“Baba yangu ananitaka kimapenzi”

Kutana na Tunu Fadhili anayesimulia jinsi baba yake mzazi alivyokuwa akimtaka yeye na wenziwe kimapenzi…na akafanikiwa kwa baadhi yao kabla yeye hajamuanika hadharani – ushahidi kwamba uhalilishaji wa kijinsia majumbani mwetu ni miongoni mwa changamoto kubwa duniani hivi sasa, na ni bahati mbaya sana kuwa jamii zetu nazo hazikuwachwa nyuma.

 


Filed under: VIDIO Tagged: familia, kibaha, ngono, tunu fadhili, unyanyasaji Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Nguzo ya sita ya mitaji ya mafanikio ni teknolojia

Huku niliko eneo la bonde la Mwakaleli, sihitaji kwenda mjini kutafuta kazi za ushauri elekezi (consultancies) ninazofanya. Huwa nawasiliana na taasisi mbalimbali zilizopo nchini na hata za nje ya nchi kuomba kazi, hususan za kuchambua na kuandika masuala anuai ya kijamii. Namaliza kila kitu na kuwasilisha juu-kwa-juu kupitia teknolojia ya mawasiliano. Ndivyo ilivyo kwa nyanja zingine za kazi mbalimbali za kibinadamu. Inatumika teknolojia.

Teknolojia yoyote ile, kwa ajili ya kazi yoyote ile, ina kazi kuu nne: kurahisisha kazi, kuleta tija au kuongeza uzalishaji (productivity), kuongeza ubora (quality improvement) na kuhakikisha usalama wa huduma na/au bidhaa tunazozalisha. Basi! Bado naamini tunapaswa kuendelea zaidi na pengine kugundua teknolojia za aina nyingi. Na kwa kusema hivyo, hakuna anayebisha kuwa teknolojia ni mojawapo ya nguzo msingi za mitaji ya mafanikio katika maisha yetu. Hongera kwa wagunduzi, na zaidi sana atukuzwe Mungu atupae vipaji vya ugunduzi ndani yetu.

Historia na Mchango wa Teknolojia Kimaendeleo

Inasadikika zama za kale (ya kale sana!) watu walikula nyama mbichi, viazi vibichi, kunde mbichi na mboga za majani mbichi. Baadaye wakagundua teknolojia ya kuwasha moto kwa kugonganisha mawe au kupekecha vipande vya miti kwa kutumia fimbo nyembamba hadi moto unawaka. Tokea hapo vimekuja viberiti, makaa, mafuta, gesi hadi umeme kwa ajili ya nishati ya kupikia, kuongeza joto, kuyeyusha chuma, kuendeshea mitambo, nk.

Ninapoandika makala haya natumia teknolojia ya mawasiliano. Niko kwenye kompyuta (mpakato), siandiki kwa kutumia kalamu ya wino na mkono, bali natumia puku (mouse) na kicharazio (keyboard) cha kompyuta huku maandishi yakijitokeza kwenye kioo cha kompyuta (monitor/screen). Baada ya kumaliza tu kuandika nitatuma mara moja kwenda gazeti la Mwelekeo kupitia anuani ya baruapepe yao (email address). Kutuma na kumfikia mhariri wa gazeti la Mwelekeo ni ndani ya dakika moja.

Zamani ningetakiwa kwanza niandike barua kwa mkono, kisha ninunue bahasha na stempu. Ningekwenda kutuma Tukuyu kwa njia ya posta umbali wa kilomita 35 tokea Mwakaleli ninakoishi. Ingenichukua takribani siku nzima kwenda na kurudi, yaani saa 24 ambazo ni sawa na dakika 1440. Badala ya kutumia dakika 1440 kwa kutuma tu makala, siku hizi natumia dakika 1 tu! Aidha, kuna rafiki yangu aliyekuwa kambi ya jeshi JKT Mlale mkoani Ruvuma ambako ujumbe wa kifo cha kaka yake kilichotokea Tanga ulichukua miezi 6 kumfikia, na akafika kwao kwa kusafiri juma zima. Alikuta kaburi limedidimia na kuota msitu wa nyasi!

Enzi za ukoloni babu yangu mkubwa katika ukoo wa Mwakatobe, hayati Lebhi Mwakaaje, inasemekana aliwahi kufanya uchuuzi wa viungo (spices) kati ya Suma (wilayani Rungwe) na Zanzibar. Mahali alipokuwa akifikia hadi sasa huitwa “Mwakiji” baada ya wenyeji kutamka jina lake hivyo, badala ya Mwakaaje. Kwenda na kurudi ilikuwa inamchukua miezi miwili. Siku hizi baada ya kuwepo usafiri wa ndege uwanja wa kimataifa wa Songwe na boti za kisasa kati ya Dar es Salaam na Zanzibar, inachukua saa 4 kwenda Zanzibar na kurudi mkoani Mbeya, badala ya kutumia miezi mwili.

Kabla na wakati wa mwanzo wa ukoloni, safari ya kutoka Dodoma kwenda Tanga ilikuwa inachukua juma zima kupitia Dar es Salaam, Unguja, Pemba kisha mnavuka bahari kwenda Tanga. Njia fupi ya sasa kupitia Chalinze na Segera haikuwepo. Vivyo hivyo, kupiga simu tulikuwa tunakwenda makao makuu ya wilaya au mkoa kupanga foleni kwenye simu za kukoroga. Kama ndugu zako wako vijijini, ujumbe wako utapelekwa makao makuu ya wilaya waliko na kuchukua takribani mwezi mzima kuwafikia. Sasa tunawasiliana kwa simu za mkononi mahali popote, muda huohuo, bila kujali umbali. Hakika tumetoka mbali na sasa teknolojia imeifanya dunia kama kijiji!

Mchango wa teknolojia ni mkubwa mno katika maisha yetu. Kazi nyingi (si zote) tufanyazo hatutumii viungo vyetu kama mikono na miguu. Tunatibiwa, tunasafiri, tunajenga, tunawasiliana, tunashona, tunaelimishwa, tunafanya biashara, tunapima muda, tunajilinda, nk.; kwa urahisi zaidi kwa kutumia teknolojia. Teknolojia imeleta madadiliko mengi na makubwa katika nyanja mbalimbali za maisha yetu. Mashine na vifaa vya kila aina na sampuli hutumika kuzalisha huduma na bidhaa kwa urahisi, kwa wingi, kwa uhakika, kwa haraka, kwa ubora, kwa faida kubwa na kwa muda mfupi.

Teknolojia ni nini hasa? Ni neno la Kiswahili tulilotohoa kutoka neno la Kiingereza la “Technology.” Technology nalo ni maneno ya Kigiriki ya “Techne” likimaanisha ufundi au ujuzi, na “logos” lenye maana ya elimu au maarifa. Kwahiyo kwa ufupi, teknolojia ni maarifa ya kisayansi ya kufanyia kazi kwa kutumia nyenzo au vifaa kwa urahisi, kwa tija na kwa ufanisi.

Sasa tunaishi katika kizazi cha ukuaji wa teknolojia kwa kasi ya ajabu. Mtu ambaye alifariki kabla ya kugunduliwa simu za mkononi, tuseme kwetu sisi kuanzia miaka ya 1990 na kurudi nyuma; endapo atafufuka ghafla hawezi kuamini tunavyowasiliana na watu wa mbali kwa vipande vidogo kama vipande vya sabuni.  Ataona kama hirizi vile au uchawi wa aina fulani.

Hata hivyo, kuna malalamiko kwamba teknolojia inatulemaza na kuchukua ajira au kazi ambazo watu tungepaswa kufanya kwa mikono yetu. Wengine wanasema teknolojia ya mawasiliano haijafanya dunia kuwa kama kijiji, eti kwasababu inatufanya tusiongee sisi kwa sisi kwa kuwa kila mtu anatingwa na simu yake ya mkononi. Tunaonywa kuwa endapo kila kitu tutatumia teknolojia kama maroboti, basi watu tutabaki kama midoli na kukosa ajira.

Wengine wanahofia kwamba hata mpira utakuwa unachezwa na midoli kwenye kompyuta! Pamoja na hayo, bado mtu atabakia kuwa bora kuliko teknolojia kwa kuwa ndiye anayegundua na kuendesha. Kompyuta au simu haiwezi kuwa na akili zaidi ya mtu aliyeitengeneza. Na kwa kusema hivyo, kamwe tusiache kuifanyisha kazi na mazoezi miili yetu ili afya na akili zetu  ziendelee kuimarika. Tuitumie teknolojia kutuendeleza na si kutulemaza.

Hitimisho

Pamoja na kuwa na nguzo zingine za mitaji ya kutufanikisha kimaisha tulizozijadili huko nyuma, yaani afya njema, fikra pevu, vipaji, rasilimali asilia na maarifa na elimu; tunahitaji sana teknolojia kwa ajili ya kuongeza tija, ubora na uwingi wa huduma na bidhaa zetu. Tulipokuwa tunaanza kuvutia wawekezaji toka nje, hususan kwenye sekta ya madini, tulitoa sababu za kutokuwa na teknolojia ya kuchimbia na kuchenjulia makinikia.

Hata hivyo, teknolojia hii ipo, inauzwa na tunao uwezo wa kununua na kuchenjua madini yetu wenyewe. Tusitafute wawekezaji na misaada toka nje, bali tutafute teknolojia ya kuzichakata, kuzisindika na kuziongezea thamani rasilimali zetu asilia. Huko China, Japan, Korea Kusini, Malaysia, Singapore, Afrika Kusini, Brazil, na nchi zingine zilizoendelea na/au zinazoendelea; hawatafuti wawekezaji na misaada, bali hutafuta kwanza teknolojia ya kuendeleza wao wenyewe nchi zao. Tusiombe kitoweo cha samaki bali tutafute teknolojia ya kuvua samaki wenyewe.

TANBIHI: Makala hii imeandikwa na Gwandumi Gwappo A. Mwakatobe, mchambuzi huru wa masuala ya kitaifa na kimataifa anayeishi Mwakaleli, Mbeya. Anapatikana kwa anuani ya baruapepe: gwandumi@hotmail.com au gwappomwakatobe@gmail.com


Filed under: JAMII Tagged: maarifa, maendeleo, mafanikio, teknolojia Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Odinga aapa kuendeleza mapambano mitaani na mahakamani

Kiongozi wa upinzani na mgombea urais kwa tiketi ya muungano wa NASA nchini Kenya, Raila Odinga, ameapa kwamba kamwe hatayatambua matokeo ya uchaguzi wa rais yaliyompa ushindi mpinzani wake mkuu, Rais Uhuru Kenyatta ambaye, kwa mujibu wa Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka (IEBC) nchini humo, alipata asilimia 54 ya kura katika uchaguzi wa Agosti 8.

Akihutubia taifa kupitia mkutano wake na waandishi wa habari jijini Nairobi hivi leo, Odinga alisema yeye na viongozi wenziwe kwenye NASA hawatakubali kile alichokiita “vifaranga vya kompyuta”, akimaanisha uongozi uliopatikana kwa matokeo ya uchaguzi yaliyokuwa yakitolewa na IEBC kupitia mfumo wa kieltroniki na ambayo ndiyo yaliyompa Kenyatta ushindi.

Kwenye hotuba yake hiyo iliyokuwa ikingojewa kwa hamu, Odinga pia amewakosoa waangalizi wa uchaguzi wa kimataifa, ambao anasema walimtolea wito wa kuyatambua matokeo ya IEBC hata kabla hayajathibitishwa.

 


Filed under: HABARI, VIDIO Tagged: IEBC, Kenyatta, Odinga, uchaguzi 2017 Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Viti maalumu ni kwa ajili ya kuwainua au kuwadidimiza wanawake?

UCHAGUZI  mkuu uliomalizika nchini Kenya umetuachia mengi ya kuyaangalia na kujifunza. Nitajaribu kufananisha machache ambayo yanatuachia mengi ya kujiuliza kwa nini sisi Tanzania yatushinde?
 
Mara baada ya Rais Kenyatta kutangazwa kuwa ndiye mshindi wa kiti cha urais alisema bila masimango ya aina yoyote kwamba iliyoshinda ni Kenya wala siyo yeye. Wakati Tanzania ilisemwa kwamba iliyeshinda ni Magufuli  na siyo mtu mwingine yeyote.
 
Vile vile Rais Kenyetta alisema kwamba wapinzani, hasa Mheshimiwa Raila Odinga, anawahitaji sana kufanya nao kazi ya kuijenga nchi yao kwa vile hata kama wao ndio wangeshinda bado kazi ilikuwa ni ileile ya kuijenga Kenya.
 
Lakini hapa kwetu, mara baada ya ushindi wa Magufuli,  wapinzani walichukuliwa kama watu wa kuja ambao rais aliyeshinda alisema hawahitaji katika shughuli zake!
 
Wakati kule Kenya rais mteule akiweka wazi kwamba shughuli za kisiasa, hata kama ni maandamano ya amani ya kumpinga yeye, ni ruksa na askari wanapaswa wayalinde kwa vile yapo kwa mujibu wa Katiba ya nchi hiyo, hapa kwetu vitu hivyo ni haramu kabisa pamoja na ukweli kwamba vinahalalishwa na Katiba ya nchi yetu!
 
Lakini kwa leo ninachotaka kukiangalia zaidi ni upendeleo kwa kina mama. Kufuatia jinsi tulivyoona kina mama wa kule Kenya wakijitokeza kupambana katika kuwania nafasi mbalimbali,  udiwani, ubunge, useneta na hata ugavana, bila kutegemea nafasi za upendeleo, nimeona kuna haja ya kuliangalia zaidi jambo hilo.
 
Nimesukumwa zaidi kuliangalia hilo na ujumbe wa maandishi niliotumiwa na James Kiemi wa Isamilo, Mwanza. Ujumbe huo unasomeka hivi:
 
“Huenda nitawaudhi baadhi ya wananchi, hasa kina mama, lakini naomba niwahakikishie kuwa nawaheshimu na kuwapenda sawia. Napendekeza nafasi za viti maalumu  ziwe maalumu kwa maana halisi ya neno maalumu. Hiyo ni kwa walemavu, wajane lakini wenye sifa ya kuelewa mambo”.
 
“Waliogombea wakashindwa lakini wakiwa na sifa za kipekee kitaifa nakadhalika. Na muda wa viti hivyo maalumu usizidi vipindi viwili kwa vile waliopata nafasi hizo kwa muda huo watakuwa wamepata uzoefu wa kutosha wa kugombea ili wakawapishe wengine nao wakanufaike”.
 
Kiemi anaongeza kwamba “Kwa mtazamo wangu tuepukane na utamaduni wa kuwaona wanawake ni vyombo, badala yake tuwaone ni watu wenye uwezo ili wakajijenge katika kujiamini wenyewe kuliko kutegemea tu fadhila, ili  waanze kuthamini zaidi vichwa vyao”.
 
Nianze kujadili hoja hiyo kwa kukumbusha kwamba kidunia ulitengenezwa mkakati shawishi wa uwakilishi wa kinamama kufikia walau asilimia 30. Lakini mkakati huo ulisuasua nchini Kenya na baadaye kugota kwenye asilimia 8.1.
 
Ila kwa sasa Bunge la Kenya linatoa asilimia 12 za viti maalumu vya kinamama na asilimia 20 kwenye seneti. Ila kule kinachotiliwa maanani ni nafasi maalumu kwa maana halisi, vijana, walemavu, wafanyakazi na makundi mengine maalumu.
 
Katika makundi hayo ni lazima jinsia izingatiwe kusudi nafasi hizo maalumu zisiende kwa jinsia moja.
 
Kwahiyo tutaona kwamba Kenya, pamoja na kulishughulikia suala la nafasi maalumu, walau wanao utaratibu muafaka unaozifanya nafasi hizo zionekane kwa nini ziitwe maalumu. Kwa upande wangu nakataa suala la umaalumu kuwaendea wanawake kana kwamba umama unamaanisha ulemavu.
 
Jambo hilo kulichukulia namna hiyo sio haki hata kidogo kwa jinsia ya kike. Na kwa mantiki hiyo naona kama nafasi hizo zitakuwa zinawadhalilisha wanawake.
 
Hata hoja ya Kiemi ya kwamba wanawake wajane wanafaa wapewe nafasi maalumu sikubaliani nayo. Sababu ujane sioni unapunguza nini katika uwezo wa mwanamke kutafakari na kuamua mambo.
 
Nitoe mfano, Profesa Anna Tibaijuka ni mjane, lakini ni wanaume wangapi wanaoweza kusema wanaufikia uwezo alionao mjane huyo kiakili? Je, naye anasitahili kupewa nafasi maalumu? Mbona kapambana na wanaume na kuwabwaga, kidunia, kimataifa, kitaifa na hata kijimbo na sasa ni mbunge wa kuchaguliwa Muleba Kusini?
 
Kwa nini Tibaijuka asiwe mfano tosha kwa wanawake wengine? Kwa nini tusimtumie mtu kama huyo kuwaamsha wanawake ili waweze kufanya mambo kwa kujiamini bila kusubiri fadhila ambazo ni kama zinaididimiza jinsia yao?
 
Wapo watu waliochangia hoja hiyo kwa njia za ujumbe mfupi wa maandishi wakisema kwamba wanawake wanaotegemea nafasi za viti maalumu kuingia Bungeni, hasa kwa upande wa chama tawala, kazi yao ni kuuponda tu upinzani huku wakipitisha kila jambo linaloletwa na serikali Bungeni kwa kusema….ndiyoo….ipiteee…bila ufafanuzi wa hoja zenye mantiki.
 
Eti wanafanya hivyo kama mtaji kusudi ukija uchaguzi mwingine warudishwe kwenye nafasi hizo hata kama watakuwa hawana faida yoyote kwa nchi na wananchi. Uwepo wao Bungeni unakuwa mzigo tu kwa walipakodi.
 
Kusema ukweli sioni kama fikra za aina hiyo zinaitendea haki jinsia ya kike. Jambo la kuondoa fikra za aina hiyo dhidi ya jinsia ya kike ni kuondoa kabisa kinachoitwa nafasi maalumu kwa wanawake, ni bora tukaiacha jinsia hiyo ijitegemee kwa kujiamini ili ikajijengee heshima isiyoyumbishwa na yeyote.
 
Nafasi maalumu, kama nilivyoonesha hapo juu, zingeachwa zibaki kwa watu walio na mahitaji maalumu, sanasana walemavu. Kumweka mwanamke kundi moja na mlemavu sio kumtendea haki hata kidogo, uko ni kuidhalilisha jinsia ya kike.
 
Mikakati ya kinamama, ambayo pia na mimi naiunga mkono, ni ya kutaka usawa wa kijinsia. Sasa inawezekanaje katika usawa ukawepo upendeleo? Neno upendeleo au nafasi maalumu, vinatakiwa vipigwe vita na jinsia zote mbili katika kuuweka usawa mahala pake.
TANBIHI: Mwandishi wa makala hii, Prudence Karugendo, anapatikana kwa anwani ya barua-pepe prudencekarugendo@yahoo.com na simu nambari +255 784 989 512

Filed under: SIASA Tagged: bunge, demokrasia, jinsia, Tanzania, viti maalum, wanawake Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Anayemuamini Profesa Lipumba anajidharau

ANAITWA Ibrahim Haruna Lipumba. Ni mwanasiasa. Kupitia kazi hii adhimu ya siasa, anajulikana vema kuwa mmoja wa wagombea maarufu wa nafasi ya urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tangu siasa za vyama vingi ziliporudishwa katika jamhuri mwaka 1992.

Amegombea nafasi hiyo mara nne – 1995, 2000, 2005 na 2010. Na mara zote akiwa ameteuliwa na Chama cha Wananchi kinachojulikana pia kwa jina la Civic United Front (CUF).

Jina lake linatangulizwa na neno “profesa” ikiwa na maana “akistahili” kuitwa Profesa Ibrahim Haruna Lipumba. Neno profesa, linalobeba herufi saba, linawasilisha wasifu wa mtu mwenye kiwango cha juu mwisho kielimu.

Profesa ni neno linalotumika kumtambulisha mtu aliyebobea katika masuala muhimu yanayohusu maendeleo ya mwanadamu.

Huyu Ibrahim Haruna Lipumba ni profesa wa masuala ya uchumi, fani ambayo umuhimu wake unajieleza bayana. Uchumi ni suala lenye mfungamano hasa na maisha ya kila siku ya mwananchi. Inasemwa na wajuzi kuwa uchumi ndio sekta kiongozi katika kumjenga mwanadamu.

Profesa Lipumba ni msomi. Kazi zake zikipigiwa mfano kwa namna zilivyoashiria kuelezea tatizo fulani linalogusa utaratibu wa kumpatia mwanadamu maendeleo. Anajadili tatizo na hatimaye kutoa ufumbuzi.

Isitoshe, profesa Lipumba anatajika mpaka viunga vya kiutendaji vya Umoja wa Mataifa (UN) pamoja na asasi za kilimwengu zinazohusu jukumu la kutoa utaalamu wa ushauri katika uendeshaji sera za kifedha na uchumi kwa ujumla wake.

Asasi kama Benki ya Dunia au World Bank (WB) na Shirika la Kimataifa la Fedha liitwalo kwa Kiingereza the International Monetary Fund (IMF) anafahamika kwa kazi za kisomi. Ndio kusema kuwa mtu atendae kazi mpaka zikavuta akili za wanataasisi hizo, huwa anatambuliwa kama mtaalamu au gwiji muhimu wa eneo fulani.

Kutokana na ukweli huo, Profesa Lipumba, nataka kuamini, hakuhangaika kupenya kuwa mwanasiasa, kama ni kweli alitamani mwenyewe kuwa.

Hwenda hadhi hiyo ya usomi wa kiwango cha juu ndiyo ilipenya ndani kabisa mwa fikra za viongozi wakuu wa CUF hata kukubali rai ya “rafiki wema” waliopenda akubaliwe kuwa mgombea urais wakati wa uchaguzi mkuu wa 1995.

Simulizi zinasema hao rafiki wema walipeleka rai yao baada ya kupata khabari kuwa uongozi wa CUF unahangaika kupata au haujapata mtu wa kumpa kijiti ili kuwakilisha chama hicho katika kinyang’anyiro cha urais nchini akipambanishwa na wanasiasa magwiji.

Hadhi na yanayotokea

Inawezekana viongozi wa CUF wanajuta. Kwa viongozi hao waliokuwa pia waasisi wa chama na hasa fukuto la siasa za mageuzi, na yumkini hata wale niliowaita “rafiki wema” kuwa katika majuto kipindi hiki, ni tafsiri halisi ya ninachothubutu kuita “kupotea kwa hadhi ya kisomi ya profesa Lipumba.” Ukitia tamati kunisoma, amua kunibishia kuwa angali msomi mkubwa na mtaalamu mbobezi wa uchumi.

Angalia anavotajika kwa mwaka sasa. Baada ya kukosa urais Oktoba 1995, akichukua nafasi ya tatu nyuma ya Benjamin Mkapa wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Augustine Mrema wa Chama cha NCCR-Mageuzi, alivikwa uenyekiti CUF.

Alifanikiwa kukisaidia chama kuimarika. Kilienea nchini na kuvuna ufuasi mkubwa. Kufikia Oktoba 2010, CUF kilikuwa na nguvu kubwa. Kikichukuliwa kama chama tishio zaidi kwa CCM.

Leo, CUF ilipo, imeongeza idadi ya wabunge wa majimbo. Haijapata kutokea katika historia yake kuwa na wabunge wengi Bara. Mazoea ni wawili tu. Awali Kigamboni na Bukoba. Ikaja Kilwa na Kigamboni. Ikaja Kilwa na Lindi mjini. Basi.

Leo inao Kilwa Kusini, Kilwa Kaskazini, Mchinga, Tandahimba, Mtwara Mjini, Temeke, Kinondoni na Kaliua. Kina madiwani wengi haijatokea. CUF leo inashika halmashauri kadhaa.

Mafanikio haya yamempita profesa Lipumba. Yalimpitaje? Alijiuzulu kwa hiari tarehe 5 Agosti 2015, miezi miwili kabla ya upigajikura. Tena, alijiuzulu hata baada ya kunasihiwa na uongozi pamoja na wazee wa CUF. Alipoamua, akatokomea. Punde akaonekana kwa picha alizopiga Rwanda ‘akila bata.’

CUF imepata mafanikio kwa ushirikiano na vyama vitatu katika umoja wa vyama vya upinzani vilivyoamua kushirikiana – Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA). Ni National League for Democracy (NLD), NCCR-Mageuzi na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA).

Profesa Lipumba labda hakupenda mafanikio ya CUF asiyoyachangia. Si aliyakimbia alipotelekeza chama? Alas, baada ya miezi kumi anarudi na akitaka kukalia kiti kilekile alichokiachia kwa jeuri na pupa.

Akijua chama kilishapata mbadala wa nafasi yake, akajitoma kwenye mkutano mkuu wa dharura wa kuchagua mwenyekiti. Hakualikwa rasmi, bali anasema “baadhi ya wanachama wameniita.”

Aliingia ukumbini Ubongo Plaza akilindwa na maofisa wa polisi waliobeba silaha. Amesahau Polisi walimbeba juujuu na kumvunja mkono uwanjani Mbagala Zakhem akikisakia chama kura mwaka 2005.

Ni Polisi haohao walimpiga na kumdhalilisha kwa kumsukuma kikatili alipokuwa Mtoni kwa Azizi Ali, njiani kwenda kuzuia wanachama waliokusanyika Mbagala Januari 2015. Leo wanamhifadhi asidhuriwe na wanachama wa CUF.

Wamemsindikiza kukalia ofisi kuu za Buguruni. Hatua hiyo ilifanikiwa baada ya walinzi wake kushambulia walinzi wa chama waliokuwa getini. Wakampiga mlinzi aliyeshika silaha. Wakavunja milango na kuingia ofisini.

Mpaka sasa profesa anaendesha harakati za “kuimarisha” chama hapo, huku akimlaumu Katibu Mkuu Maalim Seif kuwa ni mtoro kazini. Lakini anajua makao makuu ya chama ni Mtendeni, mjini Zanzibar. Anajua Maalim Seif yuko kule bukheri khamsa ishirini anafanyakazi.

Profesa Lipumba akatangaza kumsimamisha katibu mkuu. Akamteua Magdalena Sakaya, aliyekuwa naibu katibu mkuu Bara, kumkaimu Maalim Seif. Profesa anajua hana mamlaka ya kufanya hivyo maana hana vyombo halali vya kikatiba vya kumwezesha kubadilisha chochote.

Anajua kwa sababu ya ukorofi wake dhidi ya chama, aliitwa akikabiliwa na mashitaka, na aliposusa kikao, akavuliwa uanachama. Hii ni 26 Septemba, siku mbili tangu alipoingia kwa nguvu Buguruni akisaidiawa na Polisi. Anajua alikatia rufaa uamuzi huo kwenye mkutano mkuu.

Hivi unamuamini Profesa Lipumba leo? Unadhani ndiye yuleyule aliyejenga CUF hadi kuitwa “ngunguri” na Polisi namba moja, Omar Mahita? CUF ile iliyobuni kaulimbiu ya “Jino kwa jino?”

Kwa hivyo unaamini khasa Profesa Lipumba anaimarisha chama? Wakati ule hapakuwa na kesi CUF. Leo muimarishaji wa chama anaona fakhari wana-CUF kushitakiana katika kesi 14. Bado ungali unaamini yungali msomi mbobezi wa uchumi?

Umesoma lini makala zake za uchambuzi wa hali ya uchumi Tanzania na Afrika au nchi zinazoendelea? Alikuwa hashindi wiki anazo angalau mbili. Leo kaputi. Atapata wapi nafasi wakati anasikiliza vitoto vilivyoishia darasa la saba. Bado ni profesa yule? Mjinga mie naona amebadilika sana. Unayemuamini najua unajidharau bure!

TANBIHI: Makala hii ilichapishwa kwa mara ya kwanza katika gazeti la MwanaHalisi la tarehe 14 Julai 2017.


Filed under: SIASA Tagged: cuf, Lipumba, NLD, Tanzania, Ukawa, Zanzibar Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Demokrasia na haki zinapotekwa nyara kwa gharama za amani na utulivu

Kilichotokea nchini Kenya baada ya uchaguzi mkuu wa tarehe 8 Agosti 2017, si kitu cha kuungwa mkono. Mauaji dhidi ya waandamanaji waliokuwa wakipinga matokeo ya uchaguzi sambamba na ghasia zinazofanywa na waliojiunga na maandamano hayo ni mambo yanayozidi kuliweka taifa hili la Afrika Mashariki kwenye mkwamo zaidi.

Bahati mbaya ni kuwa sababu za kutokea kwa haya si ngeni ndani ya eneo zima la mashariki, kati na kusini mwa Afrika. Ndani ya kipindi cha miaka mitatu tu, mataifa yapatayo sita kwenye eneo hili yameingia uchaguzini – Burundi Julai 2015, Tanzania Oktoba 2015, Uganda Februari 2016, Zambia Agosti 2016, Rwanda Agosti 2017 na Kenya Agosti 2017 – na takribani yote yalikumbwa na matokeo yanayofanana ingawa si yote yaliyochukuwa njia moja kwenye kukabiliana na matokeo hayo. Mote watawala wamerejea madarakani na mote wapinzani wamelalamika kuwa hazikuwa chaguzi huru, haki wala za wazi.

Nchini Burundi, baada ya kuisigina katiba ya nchi yake na makubaliano ya amani ya Arusha na kulazimisha kuwania muhula wa tatu madarakani, Rais Pierre Nkurunziza, alirejea madarakani kwa asilimia 69 ya kura. Vyama vikuu vya upinzani viliugomea uchaguzi huo.

Kabla na baada ya uchaguzi huo, taifa hilo limeshuhudia maandamano, machafuko na mauaji ya hapa na pale, huku maelfu wakiikimbia nchi yao kuelekea mataifa jirani. Upinzani rasmi unaendelea kutoa matamko ya mara kwa mara dhidi ya utawala na baadhi ya mataifa ya nje yameiwekea nchi hiyo vikwazo.

Nchini Tanzania, Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) ulimsimamisha aliyewahi kuwa mwanachama wa ngazi za juu wa chama tawala (CCM), Edward Lowassa, kupambana na mwanachama asiyekuwa na mizizi mirefu ndani ya chama hicho, John Magufuli, katika uchaguzi wa Jamhuri ya Muungano, na matokeo yake Magufuli akatangazwa ushindi kwa asilimia 58.6, huku UKAWA ukiamini kuwa mgombea wao ndiye hasa aliyeshinda, lakini matokeo yakabadilishwa kwa manufaa ya chama kilichotawala kwa zaidi ya nusu karne, CCM.

Hata hivyo, katika uchaguzi wa Zanzibar, hali ilikuwa tafauti kabisa. Chama cha upinzani, CUF, kinasema CCM ilishindwa kabisa kubadilisha matokeo licha ya kukaa siku tatu nzima kukusanya na kuhakiki kura zisizofika 600,000 na hatimaye Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi, Jecha Salim Jecha, akaufuta uchaguzi huo tarehe 28 Oktoba 2015 na kisha kumrejesha madarakani Dk. Ali Mohamed Shein kwa asilimia 91.8 kupitia kilichoitwa ‘uchaguzi wa marudio’ wa Machi 2016 uliosusiwa na vyama vikuu vya upinzani.

Baada ya uchaguzi kumalizika na Magufuli kujiimarisha madarakani, kuna jitihada kubwa kabisa za utawala wake kuuwa upinzani na yumkini kwa mahisabu ya kutokukumbana na yaliyojiri mwaka 2015 ifikapo uchaguzi wa 2020. Viongozi kadhaa wa upinzani wamekamatwa, kupigwa, kuteswa, kufungwa, kunyang’anywa ama kuharibiwa mali zao na hata vyombo huru ya habari vinatishwa.

Kwa upande wa Zanzibar, kabla na baada ya Dk. Shein kurudi madarakani, kulitanda visa vya kamatakamata, pigapiga, na kuwekwa watu ndani kwa muda usiojuilikana, huku baadhi ya mataifa ya nje yakiweka vikwazo laini na upinzani unaoshikilia kutokuitambua serikali ya Dk. Shein ukitoa matamko ya hapa na pale dhidi ya utawala huo.

Lakini lazima kutaja hapa kuwa chama kikuu cha upinzani, CUF, ambacho kinaamini kuwa kilishinda tena uchaguzi wa Oktoba 2015, sasa kimeingizwa kwenye mgogoro mkubwa kabisa ambao una kila dalili za kusimamiwa na vyombo vya dola na ambao unaweza ukaififisha nafasi ya wapinzani kusimama tena imara dhidi ya utawala mwaka 2020.

Nchini Uganda, ambako Rais Yoweri Museveni amekuwa madarakani kwa zaidi ya miongo mitatu sasa, alitangazwa mshindi wa asilimia 60.62 kwenye uchaguzi wa tarehe 18 Ferbruari 2016, ikiwa ni mara ya nne mfululizo kumshinda mpinzani wake mkuu, Kizza Besigye. Upinzani unasema Besigye alishinda lakini kwa mara nyengine akazuiwa na kuiongoza nchi hiyo.

Hata hivyo, tafauti na wapinzani wenzake wa mataifa mengine ya Afrika Mashariki, Besigye aliamua kujitangaza na kuapishwa kuwa rais wa Uganda, kisha akakamatwa na kuwekwa ndani kwa uhaini. Lakini nako pia, kabla na baada ya uchaguzi wenyewe, kulikuwa na kamatakamata, pigapiga na fungafunga dhidi ya wapinzani.

Nchini Zambia, Edgar Lungu alirejea madarakani kwa ushindi wa asilimia 50.35 dhidi ya 47.63 za mpinzani wake mkuu, Hakainde Hichilema, ambaye naye ana uhakika wa ‘kuibiwa’ kura kwa maslahi ya watawala.

Upinzani nako unaandamwa kabla na baada ya uchaguzi huo wa tarehe 11 Agosti 2016 kwa vipigo, kamatakamata na vifungo. Ndio kwanza Hichilema ametolewa juzi jela alikokuwa anasubiri kesi ya uhaini dhidi yake, kosa lake likiwa kushindwa kuupisha msafara wa magari ya Lungu.

Hadithi ya Rwanda haistahiki hata kusimuliwa kwa upana wake, si kwa sababu haina mengi ya kusimuliwa, bali kwa kuwa ni shida kuchaguwa cha kusimulia kwa namna ilivyojengeka.

Katika taifa ambalo kuwa mpinzani wa kweli ni sawa kujiandikia hati ya kifo, mateso na ukandamizwaji, si ajabu kuwa kila uchaguzi, mgombea wa chama tawala hupata asilimia 90 kwenda juu.

Mwaka 2003, Paul Kagame alipata asilimia 95, mwaka akashuka kidogo kwa asilimia 95 lakini huu wa tarehe 4 Agosti 2017 akapanda tena hadi asilimia 98.7, kwa mujibu wa Tume ya Uchaguzi.

Kabla na baada ya uchaguzi, Rwanda hubakia kuwa ile ile. Machache hubadilika kwenye taswira ya kisiasa, ikiwa yapo.

Uchaguzi wa mwisho wa Kenya wa tarehe 8 Agosti 2017 umerejesha hali ile ile iliyozoeleka kwenye mataifa ya Afrika Mashariki – walio madarakani hawawezi kurejea kosa la kushindwa kwenye uchaguzi waliouandaa wenyewe.

Inaonekana ni kama kwamba kile watawala wanachokiona ni kosa lililowahi kufanyika Zambia mwaka 1991 alipoangushwa Kenneth Kaunda na hapo Kenya penyewe mwaka 2002, ambapo Uhuru Kenyatta akiwa chama tawala cha wakati huo, KANU, alishindwa na mgombea wa muungano wa upinzani aliyeikimbia KANU, Mwai Kibaki, hakipaswi kujirejea milele.

Huenda kweli, watawala katika eneo la kusini, kati na mashariki mwa Afrika wanafanya kazi nzuri ya kuzijenga nchi zao na wanakubalika sana na wapigakura kiasi cha kurejeshwa madarakani kila mara wanapofanya uchaguzi.

Lakini pia inawezekana kuwa watawala hawa wamejiimarisha sana kwenye taasisi na mifumo ya kidola kiasi cha kwamba kura za wananchi hazimaanishi chochote. Ni bahati mbaya sana kwamba huu wa pili unaonekana kuwa uhalisia zaidi.

Sikusudii kuhukumu kuwa Tume ya Uchaguzi ya Kenya (IEBC), ambayo imesifiwa na waangalizi wa ndani na nje kwa kufanya kazi yake kwa weledi mkubwa licha ya changamoto za hapa na pale, imejigeuza kuwa moja ya taasisi ya kidola ambazo amri kuu inatoka kwa mtawala.

Lakini pia sitaki kuhukumu kuwa muungano wa upinzani wa NASA unadanganya kwenye madai yake ya kuibiwa kura kwa mara nyengine.

Ninachokiona ni kuwa tabia inayojengeka kwenye mataifa yetu, hata baada ya takribani miaka 30 ya kuijaribu demokrasia ya vyama vingi, inaakisi ukweli kuwa demokrasia hii imetekwa nyara na watawala, ambao wanatumia bango la amani na utulivu kama kisingizio cha kuendelea kuwapo kwa madarakani.

Kwa maslahi ya kutunza amani, wapinzani visiwani Zanzibar wanaendelea kumalizwa na matumaini ya mabadiliko kuvunjwa kabisa. Kwa tamaa kuwa utulivu ndio njia na shabaha ya maendeleo, wapinzani Uganda nao ni hivyo hivyo. Yayo yanaweza kusemwa kwa kwengineko.

Mataifa ya Magharibi, ambayo yanahusika pakubwa na hili dubwashikana liitwalo ‘demokrasia ya vyama vingi’ ni kama kwamba nayo yameamua kuwa yalifanya kosa kushawishi kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi, na sasa kisirisiri yanaungana na watawala wanaoikandamiza demokrasia kwa kuwa tu makampuni yao ya kibiashara yanapata kuvuna rasilimali kirahisi chini ya mifumo iliyopo.

Ninapoangalia kufeli kwa kile kilichoitwa “Mapinduzi ya Arabuni” kuanzia Tunisia, Libya, Yemen, Syria na kwengineko, naona imesharasimishwa sasa kuwa demokrasia si jambo muhimu kwa mataifa hayo na yetu ya Afrika, na hivyo muelekeo wa siasa za kilimwengu sasa ni kuiteka nyara demokrasia changa iliyokwishaanza kuchipuwa kwa maslahi ya kulinda amani na utulivu unaoambiwa upo.

TANBIHI: Makala hii ilichapishwa kwa mara ya kwanza katika gazeti la Mwelekeo la tarehe 14 Agosti 2017.


Filed under: KALAMU YA GHASSANI Tagged: Burundi, Kenya, Rwanda, Tanzania, uchaguzi wa kenya 2017, Uganda, Zambia Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Akina Mnyaa, Khalifa na wenzao hawatuwakilishi Wapemba

Hii si mara ya kwanza kwa Chama cha Wananchi (CUF) kujikuta kwenye mgogoro unaokimomonyoa ndani kwa ndani na kisha kikainuka imara kusonga mbele, lakini lazima tuseme wazi kuwa mgogoro wa safari hii si kama mingine ya nyuma na kuna wasiwasi kuwa kinaweza kushindwa kuvuuka salama usalimini.

Katika mengi yaliyoibuka ndani ya mgogoro huu mkubwa, leo nataka nizungumzie kitu kimoja tu – nacho ni hawa waliojiunga na timu ya Profesa Ibrahim Lipumba kutokea visiwani Zanzibar, ambapo ukiziangalia sura zote zilizokwishajitokeza waziwazi hadi hivi sasa, unachoweza kukiona ni kisiwa cha Pemba.

Nassor Seif Amour, Mussa Haji Kombo, Mohamed Habib Mnyaa, Haroub Mohamed Shamis, Khalifa Suleiman Khalifa, Rukiya Kassim Ahmed na Thiney Juma Mohamed, wote wanatoka kisiwani Pemba, ambako kunasalia kuwa ngome madhubuti ya CUF na ambako daima kumekuwa kukikiadhibu Chama cha Mapinduzi (CCM).

Ukimtoa mwanajeshi Thiney Juma Mohamed, waliobakia wote wamewahi kuwa wabunge na au wawakilishi katika nyakati tafauti, huku wengine kama Khalifa wakikaa bungeni tangu uchaguzi wa kwanza wa vyama vingi mwaka 1995. Kwa hivyo, pamoja na kujitolea kwao kukubwa kukijenga chama, kwa hakika wao ndio hasa waliojengwa na CUF.

Pemba, kisiwa ambacho mimi pia ninatokea, kinatambulika kihistoria kwa upinzani wake dhidi ya watawala kisiowakubali, hata wawe na nguvu kiasi gani. Wenyewe Wapemba tuna fakhari ya kuwa kizazi cha wahenga waliopambana na kuushinda utawala katili wa Mreno baada ya karne nzima, tunajivunia kuupinga utawala wa Busaid, na hata uliofuata baadaye wa Mwingereza na kisha wa CCM.

Kwa sababu zinazofanana, kisiwa hiki kimekuwa sehemu ya mapambano ya Zanzibar dhidi ya wanachoamini Wazanzibari kuwa ni utawala wa Tanganyika kwa hadhi ya nchi yao.

Ukweli kwamba CUF iliungwa mkono na kisiwa kizima cha Pemba mara tu ilipoanzishwa, haukutokana pekee na sababu ya kuwa mmoja wa waanzilishi wake, Maalim Seif Sharif Hamad, ni mzaliwa wa kisiwa hicho, bali pia, na zaidi, ni kwa sababu kisiwa chenyewe kilikuwa kinasaka muda mrefu jukwaa la kuonesha upinzani wake dhidi ya mtawala wasiyemkubali.

Kwa nini sasa wanasiasa hawa kutoka Pemba wamekuwa sehemu ya genge linalosimama dhidi ya chama ambacho kimekuwa daima alama ya mapambano ya Zanzibar dhidi ya mtawala aliyeshiriki, kupanga na kuwahujumu wananchi wa Zanzibar kwa miaka-nenda, miaka-rudi?

Kwa nini akina Mnyaa na Khalifa, ambao walikaa muda mrefu bungeni kwa kura za Wapemba wenzao, wakafaidika kiuchumi wao na familia zao, wamegeuka leo dhidi ya maslahi mapana ya watu waliokanyaga mabega yao kujiinuwa?

Kwa nini akina Nassor Seif na Mussa Haji wawe sehemu ya mchakato wa kuipeleka CUF njia ya NCCR-Mageuzi, chama kilichowahi kuwa na nguvu sana mwanzoni mwa mfumo wa vyama vingi na kutikisa nchi kwenye uchaguzi wa 1995, lakini kikapandikiziwa migogoro ya kiuongozi na hatimaye kusambaratishwa, hadi sasa kimesalia na mbunge mmoja tu bungeni?

Kwa nini akina Thiney na Bi Rukiya wawe sehemu ya mkakati wa kuimaliza CUF, ambayo hadi mwaka 2015 ilikuwa sehemu ya Serikali ya Umoja wa Kitaifa visiwani Zanzibar na iliyowahi kuwa ya pili kwa ukubwa bungeni na kusaidia kuikaribisha Zanzibar kwenye ndoto yake ya kuwa na mamlaka kamili ndani ya Jamhuri ya Muungano?

Majibu ya maswali haya wanaweza kuwa nayo zaidi wenyewe, na pengine wataandika kujibu kwa wakati wao, lakini hawawezi kuondosha ukweli uliopo; kwamba, kwanza, wanachokifanya kiko dhidi ya Zanzibar yao na hivyo kisiwa chao cha Pemba walikozaliwa na kukulia na, pili, kwamba wao ni wasaliti dhidi ya Pemba na Wapemba.

Kwa yote mawili, hawa si wawakilishi wa Wapemba, mimi nikiwa mmoja wao. Nimezaliwa, kukulia na kufundwa ndani ya kisiwa hicho. Mbali ya kuutangatanga ulimwengu, bado nabakia sehemu ya Wapemba na Wazanzibari wanaojuwa nini tunakisimamia kwenye taswira ndogo ya Zanzibar na Tanzania, na kisha taswira kubwa ya Afrika Mashariki, Afrika na hata dunia kwa ujumla.

Ukihesabu gharama ambazo hata wao wenyewe zimeshawapata kwenye mapambano haya, ikiwemo kufungwa, kupigwa na hata kuuliwa kwa ndugu na jamaa zao wa karibu, akina Mnyaa na Khalifa hawakupaswa kabisa kuwa mahala hapa tupaitapo kwa Kipemba ‘asfala-safilina’ – yaani chini kuliko walio chini, panapohusika dhamira.

Lakini pengine swali kubwa kuliko yote ni kwa nini CUF yenyewe – kama chama – imefikishwa mahala hapa? Wengine wanasema ni kutokana na kosa la uongozi wenyewe wa CUF kuchelewa kuchukuwa hatua muafaka kutokana na masharti ya katiba yao, pale pale na wakati ule ule Lipumba alipoamua kuwaacha mkono wakati wakimuhitaji sana karibu na uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Kwao wao, laiti CUF ingelifuata kikamilifu katiba yake tangu siku Lipumba anajiuzulu mwenyewe na kwenda zake Rwanda, basi kiongozi huyo asingelikuwa tena na nafasi ya kurejea kuivuruga CUF kwa namna ambayo anafanya sasa kwa mafanikio makubwa kupitia mkono wa dola na ushirikiano aupatao kutoka kwa hawa waliaomua kujiunga na usaliti kutokea kisiwani Pemba.

Lakini kwa wanaoujuwa ukweli wa mambo, majibu si mepesi kiasi hicho. Hao wanajuwa kuwa CUF haidhuriwi kabisa na katiba yake, bali inadhuriwa na mambo matatu makubwa kwenye hili: kwanza ni msimamo wake dhidi ya uhuni uliotendeka Zanzibar tarehe 28 Oktoba 2015, siku uliyofutwa uchaguzi mkuu wa Oktoba 25.

CCM na vyombo vyake vya dola kwenye serikali zote havikuwahi kuisamehe CUF kwa jinsi chama hicho kilivyowaweka uchi katika kadhia hii nzima. Kwa CCM, chama cha CUF kinapaswa kuondoka kwenye uso wa dunia haraka iwezekanavyo kabla ya uchaguzi mwengine wowote ujao, maana aibu ya Oktoba 2015 visiwani Zanzibar hawakuweza kuifidia hadi leo.

Pili, CUF inadhuriwa na msimamo wake wa muda mrefu kuelekea mfumo wa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, kwani hiki ni chama pekee cha kisiasa ambacho kimejijenga vizuri mno katika “Siasa za Muungano” katika kiwango ambacho CCM inapoteza kila uchao kutokana na uungwaji mkono unaoongezeka kwa hoja ya CUF juu ya Muungano huo.

Hili halijaanza leo, na daima vyombo vya dola vimekuwa vikisaka njia ya kuimaliza CUF ili kunyamazisha kabisa hoja dhidi ya Muungano wenyewe. Hadi kufikia mgogoro huu mkubwa kabisa wa Lipumba, CUF ilishapandikiziwa mingine mingi huko nyuma kwa mkono wa vyombo vya dola kutokana na msimamo wake huo.

Na, tatu, CUF inadhuriwa na hatua yake ya kujiunga na Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), ambao uliitikisa sana CCM kwenye uchaguzi mkuu wa 2015, kiasi cha kwamba kwa mara ya kwanza chama hicho tawala kilikosa asilimia 60 ya kura za jumla. Kwenye hili, CUF hailengwi peke yake, bali ni pamoja na mshirika wake mkuu, CHADEMA, ambacho kimekumbwa na ukandamizaji mkubwa dhidi ya viongozi wake tangu kumalizika uchaguzi huo.

Kwa hivyo, Lipumba na wenzake hawapo kwenye nafasi ya kushinda ‘vita’ vinanavyoendelea sasa eti kwa kuwa uongozi wa CUF ulidharau kuitumia katiba yao kwa wakati tu, lakini zaidi ni kwa kuwa CCM na vyombo vya dola vinataka kuona kuwa CUF inasambaratika kabla ya uchaguzi mkuu wa 2020 ili kuyauwa kabisa madai ya chama hicho kwa uchaguzi wa 2015 Zanzibar, kuizika moja kwa moja ajenda ya Zanzibar kuhusu Muungano na ikibidi kuiuwa kabisa UKAWA.

Uongozi wa CUF unalijuwa hili na unasema mara kadhaa kuwa haupambani na Lipumba na genge lake wala haupingani na katiba ya chama chao, bali unapambana na kupingana na dola nzima iliyosimama nyuma ya genge hilo.

Ni jambo la kushangaza sana kwamba, kwa upande wa Zanzibar, genge hilo linaundwa na wanasiasa kutoka kisiwani Pemba pekee, anakotokea Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif, tena baadhi yao, muna ambao kupanda kwao ngazi kuliwezeshwa kwa hishima tu ya wanachama kwa Maalim Seif tu, na si vyenginevyo.

Siku wananchi walipoamua kuchukuwa hatua dhidi ya wanasiasa hawa kwa njia zao wenyewe kwenye kura za mchujo huko mashinani na wakaangushwa, akina Mnyaa, Khalifa, Mussa Haji, Rukia na wenzao, ndipo walipojitokeza kwa sura zao halisi. Maslahi.

Ni bahati mbaya kwamba sasa wanatumia sura zao hizo kuiuwa taasisi pekee ambayo ilitegemewa sio tu na wapigakura wa kisiwa chao, bali pia na Wazanzibari na Watanzania wengine kwa ujumla, kama jukwaa la kuisemea na kuitetea Zanzibar kitaifa na kimataifa.

Hawa ndio wale waitwao wa Kipemba: “Nalitote!” Madhali wao wamekosa ulwa ndani ya CUF, basi CUF nayo naife.


Filed under: KALAMU YA GHASSANI Tagged: cuf, Maalim Seif Sharif Hamad, mgogoro, Profesa Lipumba Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Ukraine yaondosha masanamu 1,320 ya Lenin

Ukraine imeyaondosha masanamu yote 1,320 ya mwanamapinduzi wa kikomunisti, Vladimir I. Lenin, kufuatia hatua ya serikali kuachana na alama zote za Kisovieti kwenye taifa hilo.

Kwa mujibu wa maafisa wa serikali, masanamu ya kiongozi huyo wa Bolshevik yameondoshwa kwenye kila mji na kijiji kinachomilikiwa na serikali ya Kiev ambayo iliuangusha utawala wa Rais Viktor Yanukovych unaoungwa mkono na Urusi miaka mitatu iliyopita.

Mpango huo wa kupingana na Usovieti, ambao pia ulijumuisha kubadilisha majina ya mitaa na miji, ulitungiwa sheria na Rais Petro Poroshenko mwezi Mei 2015, kwa mujibu wa gazeti la The Times la Uingereza.

Chini ya mpango huo, mitaa mingi imepewa majina ya mashujaa wa Ukraine, ingawa mtaa mmoja uliokuwa na jina la Lenin, magharibi mwa nchi hiyo umepewa jina la Lennon, kwa heshima ya Beatles.

Volodymyr Viatrovych, mkurugenzi wa Taasisi ya Kumbukumbu ya Taifa, alithibitisha kwamba kila sanamu la Lenin limeondoshwa sambamba na mengine 1,069 ya zama za Kisovieti.

Licha ya sheria hiyo, mabaki ya alama za Ukomunisti bado zimesalia kwenye eneo la mashariki mwa nchi hiyo, ambalo linadhibitiwa na waasi wanaoungwa mkono na Urusi.

Kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa, zaidi ya watu 10,000 wamekufa baada ya Urusi kutwaa udhibiti wa mkoa wa Crimea mwaka 2014.

Chanzo: Gazeti la The Independent la Uingereza la tarehe 18 Agosti 2017


Filed under: BURUDANI, HABARI Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.

Uhai wa CUF unategemea uadilifu wa mahakama

Kuna wanaohoji kwamba mgogoro uliopandikizwa kwenye Chama cha Wananchi (CUF) unaweza tu kumalizika kwa katibu mkuu wa chama hicho, Maalim Seif Sharif Hamad, kukaa kitako na aliyekuwa mwenyekiti wake, Profesa Ibrahim Haruna Lipumba, kuyazungumzia wanayotafautiana.

Mtazamo wa mazungumzo ndio unaonekana, kijuujuu, kutajwa pia na Profesa Lipumba mwenyewe, ambaye katika siku za hivi karibuni alinukuliwa akisema kuwa mgogoro uliopo kwenye chama chake hicho cha zamani umalizwe kwa mazungumzo nje ya mahakama, lakini kwa sharti kubwa la, kwanza, Katibu Mkuu Maalim Seif kumtambua yeye, Lipumba, kuwa mwenyekiti wake na, pili, kwenda Ofisi Kuu za CUF zilizopo Buguruni, Dar es Salaam, ili aende akapangiwe kazi na mwenyekiti wake huyo.

Kauli ya mazungumzo kama njia ya kutatua migogoro inavutia. Inawashawishi wengi waiangalie kama suluhu pekee. Inawaweka wengi hao kwenye bawa la Profesa Lipumba, kumuona kuwa mtu wa suluhu, mtu wa mazungumzo, mtu wa muafaka.

Wanaoshinikiza kuwa Maalim Seif azungumze na Profesa Lipumba wana hoja tatu mkononi mwao. Kwanza, ukweli kuwa njia ya mazungumzo ndio njia bora kabisa ya kumaliza tafauti baina ya wenye uhasama. Msemo wa kifalsafa hutuambia kuwa: “kinachoshindwa kutatuliwa kwa majadiliano, hakiwezi kutatuliwa kwa mapigano.”

Maana yake ni kuwa mapambano, kama haya yanayoendelea sasa kwenye CUF, hayatafanikisha chochote kwa upande wowote, bali mazungumzo – endapo yatafanyika kati ya pande hizo – ndiyo yanayoweza kuumaliza mkwamo uliopo.

Hoja ya pili waliyonayo ni kuwa, hata kama pametokea hitilafu kubwa baina ya Maalim Seif na Profesa Lipumba huko nyuma, basi uhasama wao hauwezi kuwa mkubwa kuliko uliokuwapo baina ya CUF kwa ujumla wake na CHADEMA, kwa upande mmoja, na au CUF na CCM, kwa upande mwengine, ambamo mote humo muwili, Maalim Seif na Lipumba walisimamia na kuongoza juhudi zilizopelekea makubaliano yaliyokuwa na faida kwa pande zote.

Kwa upande wa CUF na CHADEMA, Profesa Lipumba, ambaye chama chake kilishawahi kuitwa CCM B na cha wapenzi wa jinsia moja na CHADEMA, alikuja baadaye mwaka 2014 kushirikiana na CHADEMA, NCCR-Mageuzi na NLD kuasisi Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA), ambao umesalia hadi leo kuwa muungano pekee madhubuti wa vyama vya upinzani dhidi ya chama tawala – CCM.

Kwa upande wa CCM, Maalim Seif alikuja kushirikiana na aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa chama hicho na Rais wa Zanzibar mwaka 2009, Amani Karume, kuasisi Maridhiano ya Wazanzibari ambayo nayo yalikuja kuzaa Mabadiliko Muhimu ya Katiba, Kura ya Maoni na hatimaye Serikali ya Umoja wa Kitaifa, ambayo ilihudumu baina ya 2010 na 2015 visiwani Zanzibar.

Hoja yao ya tatu ni kwamba, hata kama Profesa Lipumba na genge lake ni wasaliti kama unavyodai upande unaomuunga mkono Maalim Seif, bado ni upande huo wa wasaliti ambao wanapewa nguvu na kila nyenzo na vyombo vyote vya dola – polisi, ofisi ya msajili wa vyama vya siasa, ofisi ya usajili na ufilisi, tume za uchaguzi, na kila aliye chini ya dola inayoongozwa na CCM.

Kwa mujibu wa hoja hii, Lipumba na kundi lake watashinda tu hatimaye kwenye vita hivi na watajipatia wanachokitaka, kama ambavyo hadi sasa wanaonekana kufanikiwa kwa kila wanalolifanya.

Wanatoa mfano wa karibuni kabisa wa Lipumba kuwafukuza wabunge wanane na madiwani wawili wa viti maalum, na kisha hatua hiyo kubarikiwa kwa uharaka wa ajabu na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa, bunge na tume ya uchaguzi.

Kwa hoja hii, ni kwamba ili Maalim Seif aendelee kubakia salama (ikiwa kweli hadi sasa yupo salama ndani ya CUF), basi ni kumridhia Profesa Lipumba kwa kila analolitaka. Ingawa wenye hoja hii hawahakikishi ikiwa endapo Profesa Lipumba akipatiwa hilo, atasimamia hapo au atataka mengine zaidi.

Nimesema kuwa hoja ya mazungumzo baina ya kambi mbili zilizopo mahakamani hivi sasa ndani ya CUF inashawishi sana. Kama unaiingia kichwa kichwa, unaweza kudhani kuwa upande wa Maalim Seif kwenye mzozo huu ni wapumbavu sana kutokuupokea haraka mkono wa maridhiano unaonyooshwa na Profesa Lipumba.

Lakini ukweli ni kuwa hoja hii imeanza kupotea njia tangu awali kabisa, na hivyo kuamua kuijibu kuangalia mwisho wake hakuna mantiki yoyote.

Kwanza, mgogoro huu uliopandikizwa kwa jina la Profesa Lipumba hauna tafauti hata kidogo na kile kitendo cha Jecha Salum Jecha wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) kuufuta uchaguzi wa tarehe 25 Oktoba 2015. Mawili haya yana uhusiano mkubwa kwa asili, njia, lengo na hata muendelezo wake.

Kwa hivyo, kama vile ambavyo huwezi kuyajadili yaliyofuata baada ya tarehe 28 Oktoba 2015, pale Jecha alipochukuwa hatua hiyo, bila kulirejea kwanza hilo tukio lenyewe na kulipima uhalali na uharamu wake, kufaa na kutofaa kwake, ndivyo ambavyo mtu hawezi kulijadili hili la Lipumba bila kwanza kurejelea kwenye chimbuko lake.

Huwezi kuenda popote kabla yakwanya kulijadili na kulimaliza la kujiuzulu kwa Profesa Lipumba kwa hiyari yake, licha ya kuombwa sana na wenziwe akiwemo Maalim Seif kwamba asichukuwe hatua hiyo, na kisha kuja kujirejesha kwenye nafasi hiyo mwaka mmoja baadaye licha ya upinzani mkubwa wa hao hao waliomtaka mwanzo abakie.

Sharti kwanza mwenye kusaka suluhu baina ya kambi hizi mbili, amalizane na hili na uhalali na uharamu wa kitendo hicho, kufaa na kutofaa kwake. Akishamaliza hilo, ndipo sasa aje kwenye meza ya mazungumzo kusaka njia ya kwenda mbele baada ya hapo.

Pili, hoja hii ya mazungumzo baina ya Maalim Seif na Profesa Lipumba imejengwa juu ya upotoshaji kwamba mgogoro uliopandikizwa na ujio huo wa Profesa Lipumba mwaka mmoja baada ya kujiuzulu, ni mgogoro baina ya Maalim Seif na yeye, Profesa Lipumba.

Licha ya wote wawili kurejelea mara kwa mara kwamba wao kama wao wana historia ya miongo kadhaa kama marafiki wa karibu, wajengaji wa hoja hii wanakataa uhalisia huo.

Bahati mbaya ni kwamba baada ya kwishajirejesha madarakani, hata Profesa Lipumba ameazima maneno hayo hayo ya kueleza uhasama baina yake na Maalim Seif, akiwacha kabisa hoja ya msingi inayozozaniwa hapa, ambayo ni matakwa ya katiba, kwa upande mmoja, na ya kimaadili, kwa upande mwengine.

Kuliweka hili kwenye nafasi yake, ni vyema ikafahamika kuwa chimbuko la mzozo huu halimo kwenye ugomvi wa wawili hao, bali limo kwenye katiba na maadili ya kiuongozi. Profesa Lipumba aliondoka kwenye uwenyekiti wa CUF kwa hoja madhubuti ya kimaadili.

Kwamba akiwa kinara wa kupambana na ufisadi, nafsi yake ilikuwa inamsuta kujiona kuwa analazimika sasa kuungana na kumpigia debe mshukiwa mkuu wa ufisadi nchini Tanzania, Edward Lowassa. Akatumia haki yake ya kikatiba, kuiacha nafasi ya kukiongoza chama chake katika wakati ambao, kwa hakika, kilikuwa kikimuhitaji sana.

Maadili na katiba vikafanya kazi yake kwake wakati huo, ikitarajiwa kuwa maadili na katiba hiyo hiyo vingelifanya kazi tena baadaye. Haikuwa hivyo, kwa upande wake. Lakini imekuwa hivyo kwa upande wa waliompinga wakati ule alipoondoka na wanaompinga leo alipojirejesha.

Na ni kwa msingi huo huo wa maadili ya kiuongozi na katiba, ndipo ambapo roho ya dhati ya CUF inasalia hadi leo. Ndipo tamaa ya kuendelea uhai wa roho hiyo ulipo. Na, hapana shaka, hakuna mahala pengine popote ambapo roho ya maadili na katiba inaweza kuhuishwa pasipokuwa kwenye mahakama inayoutambua wajibu wake na inayotenda kazi kiadilifu.

Swali ni kwamba je, idara ya mahakama nchini Tanzania inazo sifa hizo za uhuru, usawa na uadilifu? Mpaka hapo kesi hizi zitakapoamuliwa, majibu ya uhakika hakuna aliyenayo. Hiyo ni kwa sababu, katika mifano kadhaa, muhimili huu wa kugawa haki umeonekana kuchezewa na muhimili wa dola, ingawa ipo pia mifano ambapo ulisimama imara.

TANBIHI: Makala hii ilichapishwa kwa mara ya kwanza na gazeti la MwanaHalisi la tarehe 21 Agosti 2017


Filed under: KALAMU YA GHASSANI Tagged: cuf, demokrasia, Lipumba, maalim seif, mahatma, Tanzania, Zanzibar Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Image may be NSFW.
Clik here to view.
Viewing all 854 articles
Browse latest View live