Miongoni mwa masuala yanayozuwa mizozo mikubwa visiwani Zanzibar ni umiliki na uhaulishaji wa ardhi pamoja na mali nyengine zisizohamishika, ambapo matukio mengi ya kudhulumiana yanaripotiwa. Lakini je, sheria ya ardhi inakulindaje na inawezaje pia kukuingiza mtegoni kama hukuzingatia? Fuatana na Wakili Msomi Omar Said Shaaban kwenye mfululizo huu wa Zaima Sheria, ambapo leo anaizungumzia sheria hiyo na mambo inayoambatana nayo.