Quantcast
Channel: Zanzibar Daima – Zanzibar Daima
Viewing all articles
Browse latest Browse all 854

Trump hudanganya mara 5 kwa siku

$
0
0

Rais Donald Trump wa Marekani ameshatoa madai ya uongo zaidi ya mara 1,000 tangu aingie Ikulu ya White House, linaripoti gazeti la Washington Post.

Madai hayo ni yanajumuisha kauli kadhaa kuwa Sheria ya Huduma Nafuu za Afya – maarufu kama Obamacare – iko kwenye hatua zake za mwisho na ile ambayo amekuwa akiirejea mara kwa mara kwamba alikuwa kiini cha kupuguzwa kwa bei ya ndege za kivita za F-35.

Staili ya uropokaji ya bilionea huyo na mkururo wake wa Twitter umemfanya aingie kwenye dimbwi la kauli zisizo za kweli mara 1,057 tangu aingie madarakani mwezi Januari mwaka huu, kwa mujibu wa timu ya utafiti ya Washington Post.

Hii inamaanisha kwamba anatoa taarifa zisizo sahihi mara tano kwa siku. Ameshayarejea madai zaidi ya 30 uongo angalau mara tatu.

Uongo wa kwanza unaotajwa ni ule maarufu siku ya kuapishwa aliposema umati uliohudhuria ulikuwa mkubwa kuliko ilivyowahi kutokezea kwa wengine akiwemo mtangulizi wake, Barack Obama. Uongo huu ameshaurejelea mara saba. Picha zilizochukuliwa kwenye mikusanyiko yote miwili zinaonesha ukweli tafauti.

Siku mbili tu baada ya kuingia madarakani, utawala wa Trump ukaanza kupata umashuhuri kwa kile ulichokiita “ukweli mbadala” ambao hadi leo inaendelea nao.


Filed under: BURUDANI Tagged: Donald Trump, Marekani

Viewing all articles
Browse latest Browse all 854

Trending Articles