Naendeshwa, kama kichwa cha treni
Hidogoshwa, kama yaya wa nyumbani
Hichezweshwa, kama vile punguani
Hiamka, ni mbio kutwa ni njiani
Hekaheka, za kutisha insani
Hivunjika, wananitupa jaani
Niendako, huwa mimi sikuoni
Mara huko kushoto na kuliani
Kwangu mwiko, kusema ni hilakini
Hisimama, huwa dereva yu ndani
Sijahema, keshashika usukani
Na kugoma, haingii akilini
Najihisi, ninaumia jamani
Kwenda kasi, nikawa sipati kyeni
Kwa wepesi, huruma nioneeni
Mussa Shehe
Zanzibar
Filed under: KISWAHILI KINA WENYEWE
