Quantcast
Channel: Zanzibar Daima – Zanzibar Daima
Viewing all articles
Browse latest Browse all 854

Mimi ni Profesa

$
0
0

Mimi ni Profesa, nina PhD ya Political Science
Na ng’ombe wa maziwa, na magari ya kubeba kifusi
Nyumbani kwangu hakuna vitabu, kuna nyasi

Mara ya mwisho nilisoma Chuo cha Barkley
Waendako watu teule
Nimerudi kwetu, napanda tungule

Mwezangu aliyesomea uganga
Huamka nyumbani hana hata unga
Akisema, huoneka mjinga

Mdogo wangu ni mwalimu wa skuli
Anasomesha watoto mafedhuli
Kipato chake ni sawa na kuli

Profesa mwezangu aliyesoma GDR
Akarudi nyumbani, akiwa  na ari
Ana maisha mabaya hatari

Na mwengine aliyekwenda Urusi
Akawa kwa pombe, hana nafasi
Yeye ni mkubwa, apigiwa hata pasi

Mimi profesa wa Milimani
Nishindaye hilala darasani
Mitaani naoneka kama nyani

Wanafunzi ninaowasomesha
Kila siku migomo waitisha
Wakidai posho halitosha

Kusoma kwao ni kwa kukariri
Na mitihani wafanya kwa shari
Kuwasimamia kwataka ujabari

Wakimaliza nje wanakaa
Mitaani tele wamejaa
Ukiwaona wabigwa na butwaa

Mimi profesa sifanyi research
Kwa kuogopa walio na nchi
Watanambia nawaweka uchi

Nikifanya huwa nadanganya
Ili wao wasije kunionya
Au kuninyima fungu la nyanya

Kusema naishi kiujanja
Ili nikwepe yao mikwanja
Au jela kwenda ionja

Nifanye nini, ndio suali
Nijibuni watu wa mbali
Unitoke huu udhalili

Mussa Shehe
24 Mei 2017
Bonn


Filed under: DARASA LA LUGHA Tagged: political science, profesa, uchumi

Viewing all articles
Browse latest Browse all 854

Trending Articles