Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Sharif Hamad, amefichua siri kuwa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan, aliwahi kuwa mwanachama wa CUF, akidai kwamba anaijuwa hadi nambari ya kadi ya uwanachama ya mwanasiasa huyo mwanamke wa kwanza kushika nafasi ya umakamu rais akiongeza kuwa inavyoonekana sasa Mama Samia anapambana kutaka kuwania urais wa Zanzibar mwaka 2020.
↧