Chama cha Wananchi (CUF) kisiwani Pemba kimetoa onyo kali dhidi ya aliyekuwa mwenyekiti wa chama hicho ngazi ya taifa, Prof. Ibrahim Lipumba, kwamba asijaribu kukanyaga kisiwani huko kuendesha kile kinachoitwa “kongamano la vijana” kwenye ukumbi wa Kiwanda cha Makonyo, Chake Chake, siku ya Jumamosi ya tarehe 24 Februari 2018. Chama hicho pia kimelitahadharisha jeshi la polisi, ambalo limempa ruhusa hiyo Lipumba, kwamba litabeba lawama kwa chochote kitakachotokezea. Zaidi angalia vidio hii ya Mwenyekiti wa CUF wilaya ya Chake Chake, Saleh Juma.