Kufuatia mauaji mengine ya kikatili dhidi ya diwani wake, Godfrey Luena, sasa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimewataka wanachama wake popote walipo kujilinda wenyewe dhidi ya mashambulizi yanayofanywa na watu ‘wasiojuilikana’, sambamba na kulitaka jeshi la polisi kueleza kwa nini lisitiliwe shaka kwa kifo cha Luena wa Kata ya Namwawala, wilaya ya Kilombero, mkoani Morogoro.