Quantcast
Channel: Zanzibar Daima – Zanzibar Daima
Viewing all articles
Browse latest Browse all 854

Mke atoweka baada ya kumuua mumewe kwa kisu Pemba

$
0
0

Mwanamke mmoja mkaazi wa Kizimbani, Wete kisiwani Pemba, anatafutwa baada ya kutoweka na mwanawe mchanga muda mfupi baada ya kumchoma kisu na kusababisha kifo cha mumewe.

Mkasa huo ulitokea jana nyakati za Magharibi, ambapo mashahidi wanasema mwanamke huyo ambaye alikuwa mke wa marehemu kwa zaidi miaka 20 sasa, alimfuata mumewe kwenye nyumba yake nyengine, yalikotokezea malumbano na kuishia kumchoma visu miguuni mumewe.

Taarifa kutoka hospitali ya Wete alikokimbizwa majeruhi zinasema alifariki dunia majira ya saa sita na nusu usiku, kufuatia kuvuja damu kwa wingi.

 


Filed under: HABARI Tagged: Mauaji, pemba, Zanzibar

Viewing all articles
Browse latest Browse all 854

Trending Articles