Sasa unatimia mwaka tangu Watanzania kumiminika vituoni kuchagua viongozi wao kwenye Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2015, na Maoni Mbele ya Meza ya Duara inauangazia mwaka huu mmoja na kile unachomaanisha kwa mpigakura wa kawaida: Je, kura yako imekuletea kile ulichokitazamia? Je, kipi kimebadilika kuwa vipi na kipi kingepaswa kuwa vipi? Vipi kuhusu suala la Zanzibar – limekwisha au bado lingalipo? Bonyeza hapa, kuungana na wachambuzi Jabir Idrissa, Rashid Chilumba na Malisa Godlisten wakiongozwa na Mohammed Khelef kwenye Maoni Mbele ya Meza ya Duara kutoka Idhaa ya Kiswahili ya Deutsche Welle.
Filed under: Habari Mchanganyiko Tagged: Tanzania, uchaguzi, Zanzibar
